Rais
John Magufuli ametoa mwezi mmoja kwa taasisi za Serikali na watu
binafsi wanaodaiwa Sh 41.4 billioni na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
kuhakikisha wanalipa fedha hizo.
Magufuli ametoa maagizo hayo leo Alhamisi Mei 17, 2018 alipokuwa akizindua kituo cha uwekezaji cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), jijini Dar es Salaam.
Ametoa maagizo hayo baada ya Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi (CDF), Venance Mabeyo kumuomba kiongozi mkuu huyo wa nchi
kusaidia kulipwa kwa madeni hayo.
Awali, Mabeyo alimueleza Rais
kuwa changamoto waliyonayo ni kutolipwa madeni na watu wanaofanya nao kazi.
Amesema kupitia Suma JKT
walitengeneza na kukopesha watu mbalimbali na matrekta yenye thamani ya
Sh40bilioni na zilizolipwa ni Sh2 bilioni na kubaki deni la Sh 38bilioni.
Ameeleza pia Suma JKT wanaolinda
taasisi za Serikali wanadai Sh 3.4 billion, hivyo kufanya madeni
hayo kwa Sh 41.4 billioni.
"Tunaomba utusaidie kutia
msukumo katika hili kwa sababu taasisi za Serikali zina lugha ya tutalipa tu
endeleeni na ulinzi tu" amesema Mabeyo.
Mabeyo amesema kuwa kutokana na hali
hiyo wanashindwa kuwalipa pamoja na gharama nyingine za kujikimu.
"Waziri wa Ulinzi,
Katibu mkuu wa wizara ya Ulinzi waandikieni barua na mnitumie nakala ili niwe
nafuatilia watakapokuwa wameanza kulipa. Nataka fedha hizo zipatikane ili
ziweze kutumika kujenga viwanda vingine ."amesema Magufuli akijibu maombi
ya Mabeyo.
"Mtu anaanzaje kuacha kulipa
fedha ya jeshi, hii ni dharau kubwa, raia wadharauliwe
na Jeshi pia?”
“Niwaombe wote wanaodaiwa madeni kwa
kuchukua matrekta, mimi niwape mwezi mmoja. ndani ya mwezi mmoja wawe wamelipa,
baada ya mwezi mmoja vyombo vyote vya ulinzi na usalama vianze kuwasaka
wote.”
Katika hatua nyingine; Magufuli
ameagiza kuwa apelekewe majina ya maofisa waandamizi wa jeshi wastaafu ili
awateue kwenye bodi mbali mbali.
"Nileteeni majina yao kwani
napata shida kuteua viongozi wa bodi kutokana na tatizo la uadilifu wao. Lakini
hawa bado wana uadilifu na nidhamu ya kutosha na bado vijana ambao sidhani kama
yupo atakayekataa nikimteua atusaidie,” amesema.
No comments:
Post a Comment