HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday 1 June 2016

HUU NDIO MKASA MZIMA WA WATU 8 WALIOCHINJWA AMBONI TANGA. UTATA MKUBWA WABAINIKA......



MAUAJI ya Watanzania kwa njia ya kuchinjwa yanaendelea kushika kasi baada ya usiku wa kuamkia jana wakazi 8 wa kitongoji cha Kibatini, kata ya Mzizima jijini Tanga kuuawa kwa kuchinjwa shingo na watu wasiojulikana.



Watu hao ambao inadaiwa kuwa ni majambazi walivamia usiku wa kuamkia jana kwa kuvunja milango ya nyumba tatu ambazo wakazi hao walikuwa wamelala na kuwachinja kisha kuiba biskuti, mchele na sukari na kutokomea navyo kusikojulikana.

Wauaji hao inadaiwa wana uhusiano na wahalifu ambao wamekuwa wakijificha ndani ya mapango ya Majimoto na kujihusisha na matukio kadhaa cha uvamizi ili kupora vyakula na kusababisha mauaji ya wakazi wa Jiji la Tanga, ikiwamo katika duka kuu la Central Bakery mwishoni mwa Aprili mwaka huu.

Mmoja wa shuhuda wa mauaji hayo, Kea Leonard (70) ambaye pia ni mkazi wa Kibatini, katika mahojiano jana alisema wanaamini kwamba chanzo cha mauaji ya wenzao ni kulipiza kisasi.
“Wiki iliyopita majira ya saa tano asubuhi hapa tulikamata vijana saba kati ya wanane wenye umri wa kama miaka 13 ambao walikuwa wakiranda randa hapa kitongojini ili kutafuta namna ya kuvuka mto kwenda ng’ambo ya pili na ndipo mmoja wao alipotutoroka,” alieleza Leonard na kuongeza “Watoto hao tulipowaweka chini ya ulinzi na kuwahoji tukaanza kuwatilia shaka hivyo mwenyekiti aliamua kuripoti Polisi na ndipo hao wakawachukua kwa ajili ya mahojiano na hatukufuatilia tena kujua kwamba waliachiwa au la kwa sababu hao watoto sio wenyeji wala wakazi wa eneo hili.”

Aliongeza kwamba wakati wahalifu hao wanavamia nyumba ya mjumbe wa serikali ya kitongoji kabla ya kumtoa nje walisikia mmoja wa watu hao akimhoji kuhusu mahali walipopelekwa watoto saba.

Diwani wa Kata ya Mzizima, Fredrick Charles akizungumza na waandishi wa habari na kuthibitisha kwamba kati ya watu waliokufa mmoja ni Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Mleni uliopo kwenye kata hiyo.

“Hali ya usalama hapa kwetu Mzizima si shwari kwa sababu wananchi wangu wa Kibatini wamevamiwa na kuchinjwa usiku wa kuamkia jana majira ya saa sita usiku,” alisema Chiluba. Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mleni kilichopo kitongoji hicho, Shabani Amani alisema wamepatwa na hofu kubwa kuhusu matukio hayo.

“Tunadhani kuna mapungufu katika suala la ulinzi hapa kwa sababu baada ya kutokea matukio kadhaa eneo letu hasa baada ya kudaiwa kwamba mapango waliyojificha wahalifu yako hapa jirani na kwetu kikosikazi cha mchanganyiko wa askari polisi na wa JWTZ wanafanya doria kwa saa 24 lakini tunashangaa kwa nini matukio yanaendelea,” alisema Amani.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Leonard Paul (Pichani kushoto) alithibitisha mauaji hayo. “Mei 30, mwaka huu majambazi waliokuwa na visu na mapanga walivamia kaya tatu na kuua wananchi majira ya saa saba usiku,” alisema Kamanda Paul.

Aliwataja waliouawa ni Issa Hussein (50) ambaye ni mmiliki wa kaya hiyo pamoja na kuibwa biskuti, mchele na sukari katika duka dogo. Wa kaya nyingine ni Mkola Hussein (40) na Hamis Issa (20), Hamis Issa (20) na aliyemtaja kwa jina la Mikidadi (70).
Kamanda aliwataja marehemu wengine ni Mahamud (35) ambaye ni mkwe wa Mikidadi, Issa Ramadhani (25), Kadir (25) na Salum ambao ni wachunga ng’ombe kijijini humo.

Hata hivyo, mashuhuda wa tukio hilo akiwemo mke wa marehemu Mkola aitwaye Aisha Saidi, alisema walipofika nyumbani hapo waligonga mlango na kumtoa nje Mkola na kuondoka naye.
“Nimeachwa mjane na watoto sita... Baada ya hao watu kuingia walimkamata Mkola na kumdai aeleze kwamba watoto wao saba wamepelekwa wapi na alipojibu sijui wakamtoa nje na kumkusanya pamoja na wanakijiji hao wengine na kuwachinja eti tu kwa sababu hawakutaja mahali walipopelekwa watoto,” alisema Aisha.

Katika hatua nyingine, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imesikitishwa kupokea taarifa za vitendo vya mauaji ya kikatili vinavyoendelea kutokea katika maeneo mbalimbali nchini.

“Wimbi hili la matukio ya vitendo vya mauaji na ukatili uliojitokeza kwa kufuatana mwezi Mei 2016 yanavunja haki ya kuishi ambayo ndio msingi wa haki zote za binadamu kwa ujumla wake.
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora inalaani vikali mauaji haya yote na matendo yote ya kikatili dhidi ya mwanadamu yanapotokea popote nchini,” ilieleza taarifa ya Mwenyekiti wa Tume, Bahame Nyanduga.

Tume iliishauri serikali kupitia Jeshi la Polisi ichukue hatua mahsusi kuhakikisha ulinzi wa wananchi dhidi ya mauaji na vitendo hivi, kwani jukumu la kwanza la kuhakikisha usalama wa wananchi ni jukumu la serikali. Jeshi la Polisi lihakikishe watu wote waliohusika kutekeleza mauaji haya wanakamatwa ili sheria ichukue mkondo wake, ilieleza.

Wakizungumza katika eneo la tukio baadhi ya waathirika ambao ndugu jamaa na zao wamechinjwa majira ya saa saba usiku wamesema kundi la watuhumiwa wanaokadiriwa kuwa walikuwa watu nane na kuvalia nguo nyeusi walipofika katika nyumba zao waliwaamuru akina baba watoke nje kisha kuwapeleka hadi katika vichaka kisha kuwachinja.

Tukio hilo limekuja wiki mbili tu baada ya vikundi hivyo vya uhalifu vinavyodaiwa kujificha katika mapango ya Amboni Mleni Maji moto kuchinja mbuzi 48,ng'ombe wawili na kuku zaidi ya 12 lakini Kamanda wa Polisi amekiri kuwa tukio hilo ni kubwa na kwamba jitihada za polisi zinafanywa ili kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanakamatwa na kutiwa mbaroni.

MASWALI MATANO (5) TATA KUHUSU MKASA HUU
1.   Majambazi wanaporaje biskuti na mchele…?
2.   Kama shida ni mali waliouwawa walikuwa na hatia gani..?
3.   Kwanini matukio haya hayakomi licha ya juhudi zinazotajwa na vyombo vya usalama kuwa zinaendelea..?
4.   Kwanini mpaka sasa wahusika bado ni watu wasiojulikana licha ya matukio kuendelea..?
5.   Watoto saba waliokabidhiwa kwa jeshi la Polisi wako wapi na taarifa yao kwanini haikutolewa..?


No comments:

Post a Comment