HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday 19 July 2014

CLICK HAPA KUPATA TAARIFA ZA USAJILI ULIOKAMILIKA MAJUU...!



Alvaro Morata
JUVENTUS YAMNASA RASMI MORATA

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Alvaro Morata amefanikiwa kukamilisha uhamisho wake kwenda Juventus kwa ada ya euro milioni 20.

Morata aliwasili jijini Turin jana kwa ajili ya vipimo vya afya kwa mabingwa hao wa italia baada ya kupita wiki kadhaa ya tetesi juu ya uhamisho huo. Juventus sasa wamethibtisha kumsajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 21 kwa mkataba wa miaka mitano.
Katika makubaliano ya mauzo ya mchezo huyo, Madrid watapewa kipaumbele cha kuuziwa mchezaji huyo katika misimu miwili ijayo kama wakimhitaji tena kwa ada ambayo haitazidi paundi milioni 30.
SUNDERLAND WAPEWA BORIN NA LIVERPOOL MOJA KWA MOJA.

Fabio Borini
KLABU ya Liverpool imekubalia kumuuza mshambuliaji wake Fabio Borini kwenda klabu ya Sunderland kwa ada ya paundi milioni 14. Borini mwenye umri wa miaka 23 alikuwa akicheza kwa mkopo katika klabu hiyo msimu uliopita na kuisaidia isishuke daraja.

Nyota huyo wa kimataifa wa Italia alifunga mabao 10 akiwa na Sunderland na kupelekea kuibuka na tuzo ya mchezaji bora wa mwaka anayechipukia. Borini ambaye alikuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa na kocha Brendan Rodgers wakati akitua Liverpool, alihamia Anfield akitokea Roma kwa ada ya paundi milioni 11 Julai mwaka 2012.

Hata hivyo, mshambuliaji huyo kiwango chake kiliyumba toka alipotua Liverpool na kufunga mabao mawili katika msimu wa 2012-2013 kabla ya kupelekwa kwa mkopo Sunderland.
MOURINHO ADAI KUKAMILISHA USAJILI WA MAJIRA YA KIANGAZI.

MENEJA wa Chelsea Jose Mourinho

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amesema usajili wake katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi umekamilika kufuatia kumsajili beki wa kushoto Filipe Luis kutoka klabu ya Atletico Madrid. Luis anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Chelsea baada ya viungo Cesc Fabregas na Mario Pasalic pamoja na mshambuliaji Diego Costa.

Akihojiwa Mourinho amesema wamemaliza usajili jana wakati muda rasmi wa kumalizika kwa usajili ni Agosti 31 na kuishukuru klabu yake kwa kazi nzuri sio kwasababu ya wachezaji walionunua bali kuweka rekodi kwa kusajili kwa muda mfupi.

Chelsea wamekuwa wakihusishwa na tetesi za kuwataka wachezaji mbalimbali ghali katika kipindi hiki cha kiangazi akiwemo nyota wa Real Madrid na Ujerumani Sami Khedira na mshambuliaji wa Monaco radamel falcao. Hata hivyo Mourinho amesisitiza kuwa ameridhishwa na bishara waliyofanya klabu yake katika kipindi hiki kwani tayari wameshapata wachezaji wote waliowahitaji.
LAMPARD KUTIMKIA MAREKANI.

Frank Lampard
KIUNGO mkongwe wa zamani wa Uingereza, Frank Lampard anatarajia kumamilisha usajili katika klabu mpya ya Ligi Kuu ya Soka nchini Marekani-MLS ya New York City wiki ijayo.

Klabu hiyo ilifanikiwa kumshawishi nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 baada ya mkataba wake na Chelsea kumalizika mwishoni mwa msimu uliopita.

Kwasasa lampard yuko katika likizo fupi baada ya kuitumikia timu ya taifa ya Uingereza katika michuano ya Kombe la Dunia iliyomalizika nchini Brazil. Hata hivyo kiungo huyo anatarajiwa kujiunga na klabu hiyo mwanzoni mwa msimu mpya wa MLS mwaka 2015.

LIVERPOOL YAMNUNUA LOIC REMY WA QPR 

Loic Remy
LIVERPOOL imeripotiwa kufanya ununuzi wake wa 5 kabla Msimu mpya kuanza kwa kumnunua Straika wa QPR Loic Remy.
Remy, Mchezaji wa Kimataifa wa France mwenye Miaka 27, Msimu uliopita alikuwa kwa Mkopo huko Newcastle na kufunga Bao 14 katika Mechi 26 za Ligi Kuu England.
QPR wanalazimika kupokea Pauni Milioni 8.5 na kumruhusu Mchezaji huyo aondoke kama Mkataba wake unavyotaka ikiwa Dau hilo litafikiwa.
Awali ilidhaniwa Arsenal watamchukua Mchezaji huyo ambae ameichezea France Mechi 27 na kufunga Bao 5 lakini sasa inelekea Liverpool wamechukua hatua za haraka kukamilisha Uhamisho wake.
Liverpool, chini ya Meneja wao Brendan Rodgers, tayari wameshanunua Wachezaji wanne kwa ajili ya Msimu mpya ambao ni Adam Lallana, Rickie Lambert, Emre Can na Lazar Markovic.
Kutua kwa Remy Liverpool kutaifanya safu yao ya mashambulizi kuwa mpya ikiwajumuisha Ricky Lambert na Daniel Sturridge baada ya kuwapoteza Luis Suarez alieuzwa Barcelona, Iago Aspas aliepelekwa kwa Mkopo huko Sevilla na Fabio Borini alienunuliwa na Sunderland.
BPL-LIGI KUU ENGLAND
RATIBA MECHI ZA UFUNGUZI
**Saa za Bongo
Jumamosi Agosti 16
14:45           Man Utd v Swansea [Old Trafford]
17:00           Leicester v Everton [King Power Stadium]
17:00           QPR v Hull [Loftus Road Stadium]
17:00           Stoke v Aston Villa [Britannia Stadium]
17:00           West Brom v Sunderland [The Hawthorns]
17:00           West Ham v Spurs [Boleyn Ground]
19:30           Arsenal v Crystal Palace [Emirates Stadium]
Jumapili Agosti 17
15:30           Liverpool v Southampton [Anfield]
18:00           Newcastle v Man City [St. James' Park]
Jumatatu Agosti 18
22:00           Burnley v Chelsea [Turf Moor]

No comments:

Post a Comment