HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 22 December 2017

TAMBO NA VITISHO VYAONGEZEKA UGOMVI WA KOREA NA MAREKANI, CHINA NA URUSI WAINGILIA KATI.


Korea Kaskazini imesema kuwa imefanikiwa kulifanyia majaribio kombora lake la masafa marefu ambalo linaweza kufika eneo lolote la Marekani.
Runinga ya kitaifa nchini humo imesema kuwa Pyongyang sasa imefanikiwa kuafikia azimio lake la kuwa taifa lenye nguvu za kinyuklia.
Kombora hilo kwa jina Hwasong-15 ambalo imesema ndio kombora lenye uwezo mkubwa lilirushwa katika giza mapema siku ya Jumatano.
Lilianguka katika maji ya Japan lakini liliweza kuruka juu zaidi ya kombora jingine lolote la taifa hilo .
Rais wa Marekani Donald Trump ameonya vitisho kutoka kwa mataifa Korea kaskazini na Iran katika hotuba yake katika umoja wa mataifa.
Katika hotuba yake ya kwanza katika mkutano wa umja huo mjini New York, ameonya kuwa Marekani itaangamiza Korea kaskazini iwapo italazimika kujitetea ama kuwalinda washirika wake.
Alimkejeli kiongozi wa Korea kaskazinmi Kim Jong un akisema: Yuko katika harakati za ''kujitoa muhanga''.
Korea kaskazini imefanya makombora yake kinyuklia majaribio na kukiuka maamuzi ya Umoja wa mataifa.
Iran, bwana Trump alisema ni nchi ya kifisadi na inayoongozwa kidikteta kwa lengo la kutaka kuyumbisha eneo la mashariki ya kati.
Jeshi la Marekani limerusha ndege yake ya kuangusha mabomu aina ya B-1B katika anga ya Korea Kusini kama sehemu ya mazoezi ya pamoja ya angani katika hatua inayoonekana kama onyo kwa Korea Kaskazini.
Mazoezi hayo ya kijeshi yanafanyika wiki moja baada ya Korea Kaskazini kurusha kombora ililodai kuwa ni la masafa marefu ambalo linaloweza kushambulia nchini Marekani.
Marekani awali imerusha ndege hizo zenye uwezo wa juu kuonyesha ubabe baada ya majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini au majaribio ya mabomu ya nyuklia.
Korea Kaskazini yarusha kombora 'lililoruka juu zaidi'
Taifa la Korea Kaskazini limefanyia majaribio kombora lake la masafa marefu lililoruka juu zaidi na kombora hilo tayari limeonekana kuhatarisha usalama duniani kulingana na waziri wa maswala ya ulinzi nchini Marekani James Mattis.
Jaribio hilo la kombora mapema siku ya Jumatano lilianguka katika maji ya Japan.
Liliruka kwa urefu wa kilomita 4,500 na kusafiri umbali wa kilomita 960 kulingana na jeshi la Korea Kusini.
Ni jaribio la hivi karibuni ambalo limezua hali ya wasiwasi.
Mara ya mwisho kwa taifa hilo kulifanyia jaribio kombora lake ni mwezi Septemba.
Wakati huo, kombora lake la mwisho lilikuwa la sita la nguvu za kinyuklia mwezi huo.

Urusi yadai Marekani inaichokoza Korea Kaskazini
Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov amedai Marekani ndiyo imekuwa ikiichokoza Korea Kaskazini na kuichochea kuongeza kasi mpango wake wa silaha za nyuklia.
Amepuuzilia mbali wito kutoka kwa balozi wa Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wa kuvunja uhusiano na Korea Kaskazini.
Hii ni baada ya Pyongyang kufanyia majaribio kombora jingine.
Urusi imekuwa ikisema kwamba vikwazo na hatua nyingine za kuiadhibu Korea Kaskazini haziwezi kufanikiwa. Badala yake imekuwa ikihimiza kuwepo mashauriano.
Marekani imetahadharisha kwamba serikali ya Korea Kaskazini "itaangamizwa kabisa" iwapo vita vitazuka.

Trump: Japan itayatungua makombora ya Korea Kaskazini
Rais wa Marekani Donald Trump, amesema kwamba Japan itatungua makombora ya Korea Kaskazini, kwa kutumia mitambo ya kijeshi iliyonunuliwa kutoka Marekani.
Wakati huo huo, waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe, amesema kwamba, taifa lake litatungua makombora hayo kabla ya kutua ardhini, "ikiwa hilo litahitajika".
Viongozi hao wawili, walisema hayo walipozungumza na waandishi habari wakati wa kumalizika rasmi kwa ziara ya kwanza ya kitaifa ya Bwana Trump nchini Japan.
Katika miezi ya hivi karibuni, Korea Kaskazini imerusha makombora mawili hatari juu ya mipaka ya Japan.
China yaiwekea vikwazo Korea Kaskazini
Uchina imeimarisha vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini, ambapo imetangaza usitishaji wa ununuzi wa nguo kutoka Korea kaskazini mbali na uuzaji wa mafuta kwa taifa hilo kuanzia leo na baada ya muda fulani.
Hatua hiyo inaambatana na maagizo ya vikwazo yaliyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku 11 zilizopita.
Wachanganuzi wanasema kuwa vikwazo hivyo vitaathiri sana raia wa Korea Kaskazini iwapo vitatekelezwa kwenye mpaka kati ya mataifa hayo ambao hauna doria ya kutosha.

No comments:

Post a Comment