HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 22 December 2017

SIMBA YAACHANA NA MWANJALE NA DOMINGOS MIPANGO YA SANTE KWASI YAWIVA.


Klabu ya Simba SC, kupitia kwa mwenyekiti wa kamati ya usajili imetangaza kusitisha mpango wa kuwasajili kiungo Mzambia, Jonas Sakuwaha na mshambuliaji na Antonio Dayo Domingos kutoka Msumbiji.
Hans Poppe amesema kwamba katika dirisha hili dogo Simba imeachana na wachezaji hao na kusajili mchezaji mmoja tu wa kigeni ili kuimarisha kikosi chake. 

Poppe amemtaja mchezaji aliyeachwa  kuwa ni beki Mzimbabwe Method Mwanjali na anayesajiliwa ni Mghana, Asante Kwasi kutoka Lipuli ya Iringa, akasisitiza kuwa Jamal Mnyate amekwenda Lipuli kwa mkopo.

Kuhusu mchezaji Domingos, Hans Poppe amesema mipango ya usajili wake haikukamilika.

Taarifa za awali zilidai kwa Simba ingewaacha wachezaji watatu na kusajili watatu wapya wa kigeni, wachezaji hao walikuwa ni Mghana Nicholas Gyan, Mrundi Laudit Mavugo na Mwanjali ambaye aliachwa kabla, ili kuwasajili watatu ambao ni Asante Kwasi, Sakuwaha na Domingos.

No comments:

Post a Comment