JESHI la polisi mkoani Tanga, limewahadharisha wananchi kuelekea katika
msimu wa sikukuu za Krismasi na Mwaka mpya, kujiepusha na vitendo vya uvunjifu
wa amani kama ulipuaji baruti na fataki ikiwemo kuchoma moto matairi
barabarani, kwa yeyote atakayefanya hivyo atachukulia hatua za kisheria.
Kamanda wa Polisi Mkoani hapa Kamishina
Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Edward Bukombe, amesema kwamba jeshi hilo
linapiga marufuku kwa mtu yeyote kulipua au kusababisha milipuko ikiwemo
baruti, fataki na Eksozi za magari, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria
namba 13 ya sheria ya milipuko.
“Hivyo wakazi wa mkoa wa Tanga, ni marufuku
kuchoma matairi hovyo na kulipua baruti bila kibali, kufanya hivyo ni kinyume
cha sheria, kanuni na taratibu za nchi. Hatua kali za kisheria zitachukuliwa
kwa yeyote atakae kiuka agizo hili,” alisema RPC Bukombe.
Amesema uzoefu unaonesha kuwa siku za sikukuu
watu wengi hujisahau kujiwekea ulinzi ikiwemo kuwaangalia watoto hivyo alitumia
fursa hiyo kuwakumbusha wazazi kuhakikisha wanachukua hatua za kuwalinda watoto
pamoja na nyumba zao ili wahalifu wasitumie mwanya huyo kufanya uhalifu wa
kuvunja au watoto kupotea mitaani.
Kamanda Bukombe amesema kwamba jeshi hilo
limejipanga kuhakikisha kuwa wananchi wanasherehekea sikukuu hizo kwa amani na
utulivu bali aliwakumbusha kuzingatia taratibu za kumbi za burudani kufungwa
nyakati za saa 6:00 usiku na hata ibada za mkesha wa Krismasi na Mwaka mpya
zimalizike muda huo.
Katika hatua nyingine Kamanda huyo wa polisi
alisema mwenendo wa uhalifu mkoani humo, katika kipindi cha Januari hadi
Novemba mwaka 2017, umeendelea kuwa katika hali ya amani na utulivu ma hakuna
matukio yanayotishia usalama kwa wananchi baada ya kuyadhibiti kwa kushirikiana
na vyombo vingine vya dola.
Hata hivyo, alisema kwamba katika kipindi cha
Januari hadi Novemba mwaka huu, katika misako waliyoiendesha na operesheni
mbalimbali waliweza kukamata wahalifu waliofanya matukio mbalimbali ambapo kesi
za bangi zilikuwa 237 kwa bangi yenye uzito wa kilogramu 76.1 na mirungi kesi
zilikuwa 37 na uzito wa mirungi ilikuwa kilogramu 5,396.740.
Kwa upande wa wahamiaji haramu jeshi hilo
walikamata wahamiaji haramu wapatao 224 kati ya hao Wasomali walikuwa 55 na
Waethiopia walikuwa 149 na Wakenya walikuwa 20 ambao wote walifikishwa katika
vyombo vya sheria.
Kamanda huyo pia alisema kuwa katika kudhibiti ujambazi na unyang’anyi wa kutumia silaha, jeshi hilo katika kipindi hicho lilifanikiwa kukamata jumla ya silaha 14 za moto ambapo bastola zilikuwa 2, shortgun 3 na magobore yaliyotengenezwa kienyeji yalikuwa 9.
Kamanda huyo pia alisema kuwa katika kudhibiti ujambazi na unyang’anyi wa kutumia silaha, jeshi hilo katika kipindi hicho lilifanikiwa kukamata jumla ya silaha 14 za moto ambapo bastola zilikuwa 2, shortgun 3 na magobore yaliyotengenezwa kienyeji yalikuwa 9.
No comments:
Post a Comment