RAIS Kim Jong Un wa Korea ya Kaskazini amepiga marufuku
kuimba, kunywa vileo na kufanya mikusanyiko ya aina yote nchini humo wakati wa
Krismasi mwaka huu.
Kwa mujibu wa shirika la ujasusi la Korea ya Kusini
(NIS), hatua hiyo inakazia amri ya kupiga marufuku sherehe za Krismasi ya mwaka
jana (2016) ikilenga kuzuia nguvu za upinzani nchini humo hususan sasa ambapo
vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya nchi hiyo vinaonyesha kuiumiza nchi hiyo.
“Korea ya Kaskazini imeanzisha mfumo wa
jumuia za chama tawala kuripoti matatizo ya kiuchumi ya watu wanayokumbana nayo
kila siku, na imepiga marufuku mikusanyiko inayohusiana na unywaji wa vileo,
uimbaji na burudani nyingine, na imeimarisha udhibiti wa habari kutoka nje,”
lilisema NIS.
Fursa za kuitumia sikukuu hiyo kueneza uelewano na furaha
zinazidi kufifia katika taifa hilo linalodaiwa kutawaliwa kidikteta na ambalo
limepiga marufuku dini zote isipokuwa maadhimisho ya familia iliyoasisi taifa
hilo la kikomunisti. Mwaka jana, Kim aliwazuia Wakristo nchini humo kuadhimisha
Krismasi na badala yake akawataka kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa bibi yake,
Kim Jong-suk, aliyezaliwa siku ya mkesha wa Krismasi mwaka 1919.
Akiwa Mkomunisti aiyebobea, mke wa kwanza wa mwasisi wa
taifa hilo la kikomunisti, Kim Il Sung, anafahamika kwa wananchi wa Korea ya
Kaskazini kama “Mama Mtukufu wa Mapinduzi”. Miti yenye mapambo ya kuadhimisha
Krismasi huonekana katika maduka makubwa ya bidhaa jijini Pyongyang, lakini
hakuna alama zozote za kidini.
No comments:
Post a Comment