
WAANDAAJI
wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania, Kampuni ya Lino International Agency
Limited, wamesema kwamba hakutakuwa na Fainali za Taifa
za shindano la Miss Tanzania kwa mwaka 2017.
Katika taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo imeeleza
kuwa sababu kubwa ya kuahirishwa kwa shindano hilo ni ukosefu wa Wadhamini
ambao kwa njia moja au nyingine huwezesha kufanyika kwa mashindano hayo kwa
kulipa gharama mbalimbali ikiwemo zawadi za washiriki.
Aidha waandaaji hao pia wamesema kuwa kuchelewa kupata
kibali cha kuanza mchakato wa Miss Tanzania 2017, ambacho kilitolewa na BASATA
mwezi Septemba mwaka huu pia kimechangia kukosa kwasababu muda ulikuwa
umeshaenda.
Mashindano ya kutafuta warembo wa Miss Tanzania yamekuwa
yakifanyika kila mwaka na baadae kuibua mastaa mbalimbali kama Wema Sepetu,
Lulu Diva, Jokate Mwegelo na wengine wengi.
No comments:
Post a Comment