HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 22 December 2017

BAADA YA KUTAMBA KWENYE CHALLENGE HAJI MWINYI AOMBA KUONDOKA YANGA.


Beki wa kushoto wa klabu ya Yanga Mwinyi Haji ameandika barua kwa uongozi wa klabu hiyo akiomba kuondoka kwenda sehemu nyingine ambako anaamini atapata nafasi ya kucheza kwenye kikosi cha kwanza.

Mwinyi alionesha uwezo mkubwa kwenye michuano ya kombe la Chalenji iliyofanyika Kenya wakati akiitumikia timu ya taifa ya Zanzibar ‘Zanzibar Heroes’ na kuisaidia kikosi hicho kumaliza nafasi ya pili baada ya kupoteza mchezo wa fainali dhidi ya Kenya.

“Ni kweli nimeandika barua kuomba kuondoka Yanga kwa sababu sipati nafasi ya kucheza”
“Mimi ninaamini nina uwezo mkubwa lakini nashangaa nimeendelea kukaa nje kwa muda mrefu. Kama unakumbuka nimecheza mechi nyingi msimu uliopita kuanzia VPL, FA, na hata michuano ya CAF iweje leo kiwango kimeshuka hadi kukosa kabisa nafasi?”
“Namshukuru sana kocha wangu wa timu ya taifa ya Zanzibar Hemed Morocco kwa kuniamini na kuniita kwenye kikosi chake kisha kunipa nafasi, hii inaonesha ni namna gani alivyokuwa na imani na uwezo wangu.

No comments:

Post a Comment