HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 5 February 2017

SERIKALI YATANGAZA DIPLOMA KUWA KIGEZO CHA MWISHO KWA KAZI YA UANDISHI WA HABARI.



Serikali imetangaza kuwa kiwango cha chini cha taaluma anayopaswa kuwa nayo mwandishi wa habari kuwa ni 'Diploma ya Uandishi wa Habari' kwa mujibu wa kanuni za sheria mpya ya hunda za habari zilizokamilika utungaji wake hivi karibuni.

Akizungumza na wana habari leo mjini Dodoma, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo , Nape Nnauye (Pichani) amesema kuwa kanuni zimeshaundwa na zimechapishwa kwenye gazeti la serikali tangu Februari 3 mwaka huu baada ya kupokea maoni ya wadau mbalimbali.

"Tumesoma, tumechambua maoni ya wengi, wapo waliotaka iwe cheti, wengine diploma, wengine digrii, wapo waliotaka PhD na wapo waliotaka iwe mtu yeyote nayejua tu kusoma na kuandika. Serikali imesimama katikati ya maoni hayo. Sifa ya chini kabisa kwa kuanzia itakuwa ni diploma ya uandishi wa habari” Amesema Nape

Waziri Nape amesema pia kuwa sheria hiyo imeshaanza kutumika tangu Desemba 31 mwaka 2016, ambapo yeye kama Waziri mwenye dhamana alishatoa tangazo katika gazeti la serikali.

Aidha kuhusu wasio na sifa hiyo, Waziri Nape amesema kuwa serikali imetoa kipindi cha mpito cha miaka mitano ili waandishi wasiokuwa na sifa hiyo, waliopo sasa na watakaoingia kwenye taaluma hiyo, wakasome ili wawe wamepata sifa hiyo.

Amesema katika utekelezaji wa sheria hiyo, kuna taasisi ambazo tayari zipo, zitaongezewa majukumu au kazi zake kuhuishwa, pia kuna vyombo vipya vitaanzishwa na kuna taratibu mpya za kiutendaji zitaandaliwa.

Kuhusu manufaa ya sheria hiyo, Nape amesema kuanza kutumika kwa sheria hiyo ni jambo muhimu kwa tasnia hiyo kwa kuwa ni ruhusa ya kuanza kwa mchakato wa kuifanya taaluma ya habari kuwa taaluma kamili yenye sifa mahsusi na  maadili yaliyokamilika pamoja na kuwa na vyombo vya kusaidia utekelezaji wake.

Sheria hiyo ilisainiwa na Rais Magufuli Novemba 16 mwaka 2016, na siku mbili baadaye ilichapishwa kwenye gazeti la serikali baada ya muswada wake kupitishwa na Mkutano wa 5 wa bunge mwezi Novemba 2016.


No comments:

Post a Comment