HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 28 October 2016

CCM YAKEMEA UPOTOSHWAJI WA VYAMA VYA SIASA NA MAGAZETI YA NDANI NA NJE.



Chama cha Mapinduzi CCM kimekemea taarifa za upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa wakishirikiana na baadhi ya vyombo vya habari zenye lengo la kukejeli, kudhihaki, kukatisha tama, kubeza na kudhoofisha jitihada zinazofanywa na chama hicho na Serikali zake katika kuleta maendeleo kwa watanzania.

Taarifa ya Chama hicho iliyotolewa leo kwa waandishi wa habari na Mjumbe wa kamati kuu (NEC) na msemaji wa chama hicho Christopher Ole Sendeka inasema yapo magazeti mawili ya nje ya nchi ambayo hutoa makala kila baada ya miezi miwili zinazopotosha na kuandika habari zisizo za kweli kuhusu Tanzania.

Amesema mbali na magazenti ya nje pia yapo mawili ya ndani ambayo yamekuwa yakitoa makala mfululizo kwa kila wiki zinazolenga kuichafua nchi na Rais wake Dkt John Pombe Magufuli.

Ole Sendeka amesema chama hicho kinatoa wito kwa vyama vingine vya siasa nchini kutochukulia kwa wepesi maswala ya Demokrasia na mabadiliko, yasiwe ni nyimbo za kuburudisha au kutoa matumaini hewa kwa wanachama na wananchi.

No comments:

Post a Comment