HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 27 October 2016

MASUMBWI KURINDIMA DIAMOND JUBILEE KESHO, CHEKA VS MCHINA, DULLAH VS MSAUZI, PROMOTA MSANGI AAHIDI MAKUBWA.



Promota Jay Msangi (wa tatu kutoka kushoto waliokaa) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mapambano hayo.

Mabondia Dullah Mbabe na Cheng Bo Zheng wakizungumza na waandishi wa Habari kuelekea mpambano wao.
Mabondia Cosmas Cheka na Jason Bedmen wakizungumza na waandishi wa habari.
Afisa Maudhui wa Star Times akuzungumzia udhamini wao kwenye mapambano hayo.
Macho na masikio ya Mashabiki na wadau wa mchezo wa masumbwi Afrika Mashariki na kati Okt 27 mwaka hu yataelekezwa kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar Es Salaam pale Bondia mtanzania anayekuja kwa kasi nchini Dulla Mbabe anatapo mkabili Bondia kutoka nchini China Cheng Bo Zheng, kwenye pambano la kimataifa la raundi 12.
 
 Akizungumza na Mtandao huu Mkurugenzi wa mpuni ya Hall of Fame Boxing Promotion Company, Jay Msangi amesema siku hiyo pia wadau na mashabiki wa masumbwi watashuhudia mpambano mwingine wa kihistoria kati ya Bondia machachari wa Tanzania Cosmas Cheka, mdogo wake na bondia maarufu nchini Francis Ceka ambaye atapanda ulingoni kumkabili bondia kutoa Afrika ya Kusini Jason Bedmen mpambano wa raundi 10.

Bondia Cosmas Cheka alizingumza na mtandao huu juu ya maandalizi yake kuelekea mpambano huo huku swali la msingi likiwa ni… Pambano limekuja kwake ghafla Je amejiaanda vya kutosha na nini anawaahidi watanzania..???
 
“Mimi ni askari muda wote niko tayari, nafanya mazoezi kila siku, najua mabondia wengi wa tanzania ni waoga lakini mimi ngumi ni kazi yangu inayonilisha kwahiyo muda wote niko tayari, nitampiga tu, hii ni rangi tu, leo ni mweupe lakini kesho huyu atakuwa mwekundu, sisi wamakonde tuna msemo usemao madengo ntiima yaani kazi ni moyo” alisema Cosmas Cheka.

Naye Bondia Dulla Mbabe alizungumzia maandalizi yake kuelekea mpambao huo pambeni yake akiwemo bondia kutoka china Cheng Bo Zheng.
“wengi mnafahamu uwezo wangu, na mnakumbuka nilichomfanya Mada Maugo, huyu ameyakanyaga, mwenzie nilimfuata hukohuko nadhani huyu aliona na sasa ameyakanyaga mpira unadunda lakini sio kwenye matope”

Mabondia wote watakao panda ulingoni hapo Okt 28 tayari wamepima uzito na majibu kuwekwa hadharani,
Jason Bedmen kg 64.6 vs Cosmas Cheka kg 64.5
Cheng Bo Zheng kg 78.7 vs Dulla Mbabe kg 77.5
Mapambano ya utangulizi
Said Mbelwa vs Thomas Mashali
Shabani Kao vs Paul Kamata
Kurwa Bushiri vs Adamu Ngange

Mapambano hayo yataoneshwa Live na King'amuzi cha Star Times kupitia chaneli ya SIBUKA MAISHA na kurudiwa na TBC2.






No comments:

Post a Comment