HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday 18 August 2016

KAMPUNI YA TANGA CEMENT YAZINDUA KINU CHA PILI CHA UZALISHAJI WA KLINKA NCHINI




Na Said Killeo ..TANGA
Kampuni ya saruji ya Tanga Cement jana ilizindua kinu cha pili cha kuzalisha bidhaa ya klinka hatua inayotajwa kuwa itakiwezesha kiwanda hicho kuongeza uzalishaji wa malighafi hiyo muhimu katika utengenezaji wa saruji kutoka tani laki tano kwa mwaka mpaka kufikia tani milioni moja na laki mbili na nusu (1.25mil).

Akizungumza katika katika hafla ya uzinduzi wa kinu hicho, Mwenyekiti wa Bodi wa kampuni hiyo, Wakili Lawrence Masha, alisema Mradi huo ulioanza Agosti 13, 2013 unajumuisha mtambo wa kuponda mawe chokaa na udongo, mtambo wa kuchanganyia mawe chokaa na udongo, mtambo wa kusaga mchanganyiko wa udongo na mawe chokaa, pamoja na  mtambo wa kusaga makaa ya mawe.

Alisema gharama za ujenzi wa mradi huo mpaka kukamilika ni kiasi cha dola za kimarekani milioni 152 huku akiongeza kuwa majaribio ya uzalishaji wa klinka ya kwanza kutoka kinu hicho kipya yalifanyika Disemba 10 mwaka 2015.
 

No comments:

Post a Comment