Walisema mbali ya uchakavu huo unapotokea ujio wa viongozi
wa Serikali maji hutoka katika mabomba na kuwapa mashaka juu ya sababu zinazopelekea
kukosekana kwa maji kwa muda mrefu.
Alisema kuna tishio
la kuzuka kwa magonjwa ya tumbo na kichocho baada ya wakazi wote kutumia maji
ya mto kwa matumizi ya kunywa kupikia na kuongea wakiwemo wanyama.Akizungumzia
kero hiyo, Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji kata ya Magati, Kimwaga Shauri,
alisema uhaba huo wa maji kijiji cha
Mwanyumba umetokana na vijiji kuongezeka ambapo awali kijiji hicho kilikuwa
hakimo katika mradi wa maji.
“Mradi wakati ulijengwa ulikuwa wa vijiji vitatu na sasa tuko na vijiji saba jambo ambalo
linatupa wakati mgumu kuyagawa na kuzifkia kaya ikiwemo kijiji cha Mwanyumba
ambacho hakikuwemo katika mradi” alisema Shauri
Alisema jitihada za kuhakikisha maji yanapatikana kijijini
kwa kutumia mfumo wa zamu unafanyika na kuwataka wananchi kulinda vyanzo vya
maji na kuacha kukata miti .
No comments:
Post a Comment