
Kutokana na hali hiyo, Rais Magufuli
ameviagiza vyombo vya dola kuwasaka kwa nguvu zote, watu waliohusika na mauaji
hayo na kuhakikisha wanatiwa mbaroni ndani ya kipindi kifupi.
Akitoa salamu za pole nyumbani kwa
wafiwa jana, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, alisema Rais Magufuli
ameguswa na tukio hilo na kusema umefika wakati wa wananchi kumwabudu Mungu ili
maovu kama hayo yasitokee.
“Wakati nakuja huku, Rais Magufuli
amenituma nimfikishie salamu zake za rambirambi kwa ndugu, jamaa na marafiki
mliofiwa.“Ameagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha vinawasaka na kuwatia
mbaroni watu waliohusika na tukio la kinyama ili wafikishwe kwenye vyombo vya
sheria,” alisema.
Alisema Rais Magufuli ametaka
wahusika wote wakamatwe ndani ya kipindi kifupi, kwa sababu mauaji ya aina hiyo
hayakubaliki hata kidogo.
Samia alisema Rais Magufuli
amewataka wananchi kumcha Mungu kwa kuwa wakishika imani na kumwabudu maovu
yatapungua.
Alisema jamii ya wacha Mungu haina
maovu mengi kama hayo.Kuwasili kwa Samia katika msiba huo, kuliamsha vilio
vingi kutoka kwa wananchi waliokuwapo.Samia alitembelea sehemu ambayo ujenzi wa
makaburi matano ulikuwa unaendelea kwa gharama za Halmashauri ya Wilaya ya
Sengerema.
Miili ya watu hao watano inatarajia kuzikwa leo kijijini
Sima.
No comments:
Post a Comment