HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 19 May 2016

"KIMBEMBE" PAMOJA NA KUJIUZULU MKWASA AMWITA CANAVARO STARS.



Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Boniface Mkwasa ametaja kikosi chenye majina ya wachezaji 26 kitakachoingia kambini kujiandaa na mechi dhidi ya Kenya pamoja na ile ya kufuzu kwa ajili ya fainali za Mataifa ya Afrika dhidi ya Misri.
 
Katika kikosi hicho nahodha wa zamani, Nadir Haroub amerudishwa kundini licha ya awali kutangaza kujiuzulu kuchezea timu ya taifa. Haroub ameitwa kuziba pengo la Kelvin Yondani ambaye anatumikia adhabu ya kadi mbili za njano na hivyo kuikosa mechi ya Misri Juni 4.Ikuumbukwe mapema mwaka huu Canavaro alitangaza kustaafu soka la kimataifa kwa kutoichezea Taifa Stars baada ya kuvuliwa kitambaa cha unahodha na kukabidhiwa Mbwana Samatta. Baadae beki mwingine wa Stars Aggrey Morris alitangaza pia kustaafu kuichezea Stars

Kikosi cha Taifa Stars kitaingia kambini tarehe 23 kujiandaa na mchezo wa kirafiki dhidi ya Kenya utakaochezwa tarehe 29 Mei jijini Nairobi.Baada ya hapo Taifa Stars itarejea Dar kukamilisha maandalizi ya kuivaa Misri katika mchezo ambao inahitaji ushindi wa angalau mabao matatu kuweka hai matumaini ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika nchini Gabon mwakani.

KIKOSI KAMILI: KIKOSI CHA STARS:
Walinda Milango: Deo Munish ( Yanga), Aishi Manula (Azam) Benno Kakolanya ( Prisons).

Walinzi: Juma Abdul, Haji Mwinyi,Nadir Haroub (Yanga ), Erasto Nyoni, David Mwantika, Aggrey Morris ( Azam), Mohamed Tshabalala (Simba), Andrew Vicent ( Mtibwa Sugar).

Viungo: Himid Mao, Farid Mussa ( Azam), Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto (Simba), Mohamed Ibrahim, Shiza Kichuya ( Mtibwa Sugar ),Hassan Kabunda ( Mwadui ), Juma Mahadhi (Coastal Union). Ismail Issa Juma ( JKU)

Washambuliaji: Elias Maguri ( Stand United), John Bocco ( Azam) Ibrahim Hajib ( Simba), Mbwana Samatta ( Genk GRC, Ubelgiji), Thomas Ulimwengu ( TP Mazembe)

No comments:

Post a Comment