
Mwanambuu alisema baada ya kupata
taarifa hizo alitoa taarifa Kituo kidogo cha Polisi Chala, askari walifika na
kuchukua mwili kwa ajili ya uchunguzi na kuanza msako dhidi ya mtuhumiwa. Akielezea
chanzo cha mauaji hayo, Mwanambuu alisema mtuhumiwa alipata taarifa kuwa
Nambasita ana uhusiano na mtalaka wake, ambaye walikuwa wameachana kipindi
kirefu.
Alidai kuwa kutokana na taarifa
hizo, mtuhumiwa alipeleka shauri la ugoni katika Mahakama ya Mwanzo Chala.
“Lakini kabla hata shauri
hilo halijamalizika, tunashangaa kuona mtuhumiwa ameamua kujichukulia sheria
mikononi, baada ya kutekeleza unyama huo alikimbia na kutokomea
kusikojulikana,” alisema.
Mtendaji wa Kijiji cha Chala,
Godfrey Mwanakatwe alisema kutokana na mazingira hayo polisi wanawashikilia
watu wanne kwa kosa la kushiriki mauaji hayo. Hatua hiyo inatokana na baada ya
wao kutoa taarifa kwa muuaji kuwa Nambasita ana uhusiano wa kimapenzi na
mtalaka wake, ambaye mpaka sasa haijulikani alipo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa,
Jacob Mwaruanda alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba, baada ya
uchunguzi wa polisi ndugu wa marehemu waliruhusiwa kuuzika mwili huo. Mwaruanda
alisema chanzo cha kifo hicho ni wivu wa mapenzi na kuongeza kuwa mtuhumiwa
alianza vizuri kwa kufuata sheria, lakini haijulikani kilichosababisha kuchukua
uamuzi huo wa kinyama.
Alisema wanawashikilia watu watatu
wakituhumiwa kushiriki mauaji hayo, kwa kutoa taarifa kwa mtuhumiwa kwamba
Nambasita alikuwa na uhusiano na mtalaka wake. Kamanda Mwaruanda aliwataka
wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi, hivyo wafuate taratibu kupata
haki zao.
No comments:
Post a Comment