MKAAZI
wa shehia ya Mtambwe Kaskazini Wilaya ya Wete Fatma Omar Hassan(28) amelazwa
katika Hospitali ya Wete kwa matibabu akiuguza majeraha aliyoyapata kutokana na
kukatwa kwa mapanga kwa wivu wa mapenzi .
Akizungumza kwa tabu na mwandishi wa
habari hizi kutokana na maumivu aliyoyapata akiwa katika Wodi ya
akinamama Hospitalini hapo , Fatma Omar Hassan alimtaja kijana aliyehusika na
kitendo hicho kuwa ni Ali Abdalla .
Aidha alikana kuwa na uhusiano
wa mapenzi na kijana huyo , licha ya kwamba amekuwa akimfuatilia kwa muda mrefu
akimtaka kimapenzi lakini hakukubaliana na matakwa ya kijana huyo .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini
Pemba Hassan Nassir Ali amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba
limetokea april 9 na Jeshi la Polisi linamshikilia kijana Ali Abdalla Ali
anayetuhumiwa kuhusika na shambulio hilo .
Kamanda Nassir alisema kuwa
mtuhumiwa bado anaendelea kuhojiwa na upelelezi ukikamilika atafikishwa
mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili .
Hivyo aliwataka wananchi kuacha
kujichukulia sheria mikononi mwao , bali waafuate taratibu kwa kuwasiliana na
Jeshi la Polisi kwa hatua za kisheria kwani lipo kwa ajili ya kulinda usalama
wa wananchi pamoja na mali zao.
No comments:
Post a Comment