HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 13 April 2016

BINTI AKATWA MAPANGA KWA WIVU WA MAPENZI HUKO PEMBA.




MKAAZI wa shehia ya Mtambwe Kaskazini Wilaya ya Wete Fatma Omar Hassan(28) amelazwa katika Hospitali ya Wete kwa matibabu akiuguza majeraha aliyoyapata kutokana na kukatwa kwa mapanga kwa wivu wa mapenzi .

Akizungumza kwa tabu na mwandishi wa habari hizi kutokana na maumivu aliyoyapata akiwa  katika Wodi ya akinamama Hospitalini hapo , Fatma Omar Hassan alimtaja kijana aliyehusika na kitendo hicho kuwa ni Ali Abdalla .

 Aidha alikana kuwa na uhusiano wa mapenzi na kijana huyo , licha ya kwamba amekuwa akimfuatilia kwa muda mrefu akimtaka kimapenzi lakini hakukubaliana na matakwa ya kijana huyo .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Hassan Nassir Ali amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba limetokea april 9 na Jeshi la Polisi linamshikilia kijana Ali Abdalla Ali anayetuhumiwa kuhusika na shambulio hilo .

Kamanda Nassir alisema kuwa mtuhumiwa bado anaendelea kuhojiwa na upelelezi ukikamilika atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili .

Hivyo aliwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi mwao , bali waafuate taratibu kwa kuwasiliana na Jeshi la Polisi kwa hatua za kisheria kwani lipo kwa ajili ya kulinda usalama wa  wananchi pamoja na mali zao.

No comments:

Post a Comment