HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 2 March 2016

CHAMA CHA CUF CHASUSIA UCHAGUZI MAZIMA UNGUJA, MPAKA WA KIJITOUPELE.



CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema licha ya kutangaza kususia uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20 mwaka huu, pia hakitashiriki uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kijitoupele, mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja utakaofanyika sambamba na uchaguzi wa marudio.

Uchaguzi wa Kijitoupele umeitishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) baada ya kutofanyika Oktoba 25 mwaka jana kutokana na kasoro mbalimbali.
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Umma wa CUF, Hamad Masoud, aliliambia gazeti hili jana kuwa uamuzi wa kutoshiriki uchaguzi wa marudio unafahamika na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na huo ndiyo msimamo wa chama.

Hata hivyo, pamoja na msimamo huo wa CUF, ZEC ilitangaza kumtambua mgombea Urais wa chama hicho, Seif Sharif Hamad.

Masoud alisema chama hicho hakitoshiriki uchaguzi mdogo wa marudio wa Kijitoupele kwa sababu hakijaridhishwa na uamuzi wa ZEC wa kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana ulioelezwa kujitokeza kasoro nyingi.

"Msimamo wa CUF unafahamika kwamba hakitoshiriki katika uchaguzi wa marudio wa Machi 20 sambamba na uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kijitoupele ambao umeitishwa na NEC," alisema Masoud
.
Alisema chama chake hakitoshiriki katika uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo la Kijitoupele kwa sababu unafanyika sambamba na uchaguzi wa marudio wa Machi 20 ambao CUF hakiutambui kama ni uchaguzi halali.

CUF ina jumla ya wabunge 27 katika majimbo ya uchaguzi ya Zanzibar ambao wanashiriki katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mjini Dodoma, kwa hivyo haioni shida kulikosa jimbo moja la Kijitoupele ambalo uchaguzi wake uliahirishwa Oktoba 25 mwaka jana.

Kwa hivyo NEC tunaijulisha kuhusu uamuzi wetu," alisema Masoud. Uchaguzi mdogo wa ubunge wa Jimbo la Kijitoupele unafanyika Machi 20 baada ya kuahirishwa Oktoba 25 mwaka jana na NEC kutokana na kujitokeza kwa kasoro mbalimbali. Jimbo hilo ni miongoni mwa majimbo matano mapya yaliyotangazwa na ZEC.

No comments:

Post a Comment