
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari
ofisini kwake Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa (EWURA), Felix Ngamlagosi
amesema bei ya Petroli imeshuka sh. 31 kwa lita sawa na asilimia 1.70,
Dizeli sh. 114 kwa lita sawa na asilimia 7.10 na mafuta ya taa kwa sh. 234 kwa
lita sawa na asilimia 13.75 ikilinganishwa na mwezi uliopita.
Ngamlagosi amesema hapa nchini kwa sasa Petroli
itauzwa Sh.1,811, Dizeli sh. 1,486 na mafuta ya taa sh. 1,465. kupungua
kwa bei hizo kwa soko la ndani kumetokana na kuendelea
kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia.
Pia amesema hakutakuwa na mabadiliko yeyote ya
bei ya petroli na dizeli kwa mkoa wa Tanga kwa mwezi huu na kwamba hiyo
imetokana na kutopokea mafuta mapya kupitia Bandari ya mkoa huo katika
kipindi cha Februari mwaka huu.
Ameongeza kuwa kwamujibu wa sheria ya mafuta
ya mwaka 2015, bei za bidhaa za mafuta zitaendelea kupangwa na soko hivyo
Ewura itaendelea kutoa taarifa za bei kikomi lengo likiwa ni kuwasaidia
wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa hiyo.
Alisema kwamba katika mabadiliko hayo,
bei za mafuta kwa mkoa wa Tanga, zitabaki zile zile za mwezi uliopita, hiyo ni
kwa sababu hakuna mafuta mapya yaliyopokelewa kwenye bandari ya Tanga.
Hata hivyo amevitaka vituo vyote vya mafuta nchini
na kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayonekana bayana
na yakionesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au
promosheni zinazotolewa na kituo husika ni kosa kuuza mafuta bila kuweka
mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa
kituo husika.
Ngamlagosi amewataka wanunuzi kuhakikisha
wanapata stakabadhi ya malipo inayoonesha jina la kituo, tarehe, aina
ya mafuta kwa lita na kwamba stakabadhi ya malipo itatumika kama kidhibiti
cha mnunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa mafuta
kwa bei ya juu kuliko bei kikomo, au yenye kiwango cha ubora kisichofaa.
No comments:
Post a Comment