HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 29 February 2016

SHAURI LA KESI YA BABU SEYA SASA KUSIKILIZWA MACHI 11 MWAKA HUU.



Baada mwanamuziki Nguza Viking (Babu Seya) na mwanae, Johnson Nguza(Papii Kocha), (Pichani Kushoto) kushindwa Mahakama ya Rufani na kukimbilia Mahakama ya Haki za Binadamu na Watu ya Afrika (AFCPHR), sasa shauri hilo limepangwa kuanza kusikilizwa Machi 11.
Ratiba ya shughuli zitakazofanyika mahakamani hapo katika vikao vyake vya kawaida, zinaonyesha kuwa Rais wa mahakama hiyo, Jaji Agustino Ramadhani, tayari amekwishaanza kuongoza vikao vya majaji wenzake kusikiliza kesi mbalimbali zaidi ya 50.

Kesi ya Babu Seya ni miongoni mwa kesi zilizopangwa kusikilizwa Machi 11, mwaka huu.Mahakama hiyo ina majaji 11 kutoka nchi wanachama wa umoja wa Afrika (AU) ambapo hukutana mara nne kwa mwaka katika vikao vyake vya kawaida.

Walalamikaji hao wanaiomba mahakama hiyo kutoa amri ya kumlazimisha malalamikiwa (Serikali ya Tanzania) kuwaachilia huru, kulipwa fidia na nafuu zingine ambazo itaona kuwa wanastahili kuzipata.Katika shauri hilo namba 006/2015, walalamikaji wanaiomba mahakama hiyo kutoa uamuzi kwamba haki zao zimevunjwa na hivyo waachiwe huru na kulipwa fidia.

No comments:

Post a Comment