MBUNGE wa jimbo la
Korogwe Vijijini, Stivin Ngonyani, maarufu kama Profesa Majimarefu, ametoa jezi
seti tano, mipira mitatu vyenye thamani zaidi ya shilingi laki 5 kwa timu ya
mpira ya vijana wa Makuyuni Wilayani Korogwe lengo likiwa ni kukuza vipaji.
Vifaa
hivyo kwa mujibu wa Mbunge huyo vimekuja kufuatia maombi ya vijana wa Makuyuni
kumtaka kusaidia ili kuweza kuimarisha timu yao na kuingia ligi ngazi ya Wilaya
hadi Mkoa.
Alisema
msaada huo hautoishia hapo lakini atapenda kuona timu hiyo inafanya vizuri ligi
ngazi ya Tarafa na kuahidi kuisaidia kwa hali na mali hivyo kuwataka kuonyesha
moyo na mapenzi na timu.
“Leo nawapeni jezi na mipira kumaliza
kilio chenu kwani nakumbuka barua yenu muloniandikia nikiwa bungeni na
mukaiacha kwa katibu wangu pale ofisini, niwaahidi kuwa mimi kama mbunge wenu
nitakuwa nanyi bega kwa bega” alisema
Majimarefu na kuongeza
“Nitahakikisha
timu yenu inaingia mashindano ya Wilaya hadi mkoa na mimi kuwa mlezi wenu na
musisite kunieleza kwa lolote” alisema
Kwa
upande wake Kocha wa timu hiyo, Mbaraka Kiondo, alimshukuru mbunge huyo na
kusema kuwa msaada wake huo aloutoa utatumika kama ilivyo na kumuahidi kuwa
hawatamuangusha katika mashindano ya ligi.Alisema awali walikuwa wanatumia
mipra mmoja huku wakiwa hawana jezi na badala yake kila mchezaji alikuwa
anatumia fulana yake jambo ambalo lilikuwa kero wakati wa uchezaji na
kutoelewana.
“Mheshimiwa Mbunge hatuna la kukulipa na
hatuna la kusema kwani hatujui tuanze wapi ila nimalize kwa kusema asante sana
na Mungu ndie atakakulipa na kukubariki” alisema Kiondo
Aliwataka
wachezaji wake kuzingatia muda wa kufanya mazoezi baada ya kupata vifaa hivyo
na kuwataka kupiga kambi ili kushikilia usukani wa ligi hiyo ngazi ya Tarafa na
msimu wa ligi kuingia ngazi ya Wilaya.
No comments:
Post a Comment