HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 2 March 2016

ANASWA AKIJARIBU KUWAHONGA POLISI MIL 5 TANGA...

POLISI mkoani Tanga inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa askari wa upelelezi.Wanaoshikiliwa ni mkazi wa mjini Korogwe, Richard Ruther ‘Mhina’ (40) ambaye ni mmiliki wa bastola namba GBT 552 inayodaiwa kufanya unyang’anyi na kisha kusababisha mauaji ya askari na raia mmoja.

Mwingine ni Hamidu Rajabu ‘Wad’ (44) mkazi wa Kabuku wilayani Handeni ambao kwa pamoja wanadaiwa kutoa rushwa ya Sh milioni tao kuzuia askari kuendelea na upelelezi kuhusu tukio la ujambazi lililotokea Februari 14 mwaka huu Barabara ya sita jijini Tanga na kusababisha kukamatwa kwa bastola hiyo inayomilikiwa na Mhina.


Kamanda wa Polisi mkoa, Mihayo Msikhela alisema jana kwamba, watu hao walikamatwa jijini Tanga Februari 26 mwaka huu saa 10.50 jioni wakiwa ndani ya ofisi ya Mkuu wa Upelelezi baada ya kuwekewa mtego na askari. (PICHA NI MAFANO)

No comments:

Post a Comment