HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 3 March 2016

TAKWIMU MPYA.. DANGOTE MTU TAJIRI ZAIDI AFRICA APANDA CHATI KWA DUNIA..



Mtu tajiri zaidi barani Afrika, Aliko Dangote wa Nigeria, amepanda katika orodha ya mabilionea duniani inayotolewa na jarida la Forbes, -utajiri wake ukifikia dola bilioni 15.4. Bwana Dangote amepanda hadi nafasi ya 51, ikilinganishwa na nafasi ya 67 mwaka 2015, alipokuwa na utajiri wa dola bilioni 14.7.
Dangote ni muasisi na mwenyekiti wa kampuni ya Dangote Cement, ambayo ni mzalishaji mkubwa wa saruji barani Afrika. Mtu wa pili kwa utajiri barani Afrika ni Mike Adenua, pia kutoka Nigeria ambaye ana utajiri wa dola bilioni 10, huku mfanyabiashara wa almasi Nicky Oppenheimer wa Afrika Kusini akishika nafasi ya tatu, akiwa na dola bilioni 6.6, kwa mujibu wa Forbes.
Matajiri hao- katika orodha ya mabilionea duniani,- bwana Adenua yupo katika nafasi ya 103, na bwana Oppenheimer katika nafasi ya 174. Bilionea kijana kutoka Tanzania Mohammed Dewji yupo katika nafasi ya 1577, akiwa na utajiri wa dola bilioni 1.1.
Kwa orodha kamili ya watu wenye 'kisu kikali' duniani, bofya hapa: http://www.forbes.com/billionaires/list/…

No comments:

Post a Comment