
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe (PICHANI) alisema tukio hilo lilitokea usiku wa
Jumatatu iliyopita katika machimbo ya dhahabu, Kijiji cha Mtoro Mtupweshi
Kamprigando.
Aliwataja
waliofariki dunia kuwa ni Salum Mfanga (44) Mkazi wa Temeke, Dar es Salaam, Yusuph Twalibu
(34) na Mariam Ramadhani (30) wakazi
wa Tanga na Hamisi Mkapira (40) wa Morogoro.
Kamanda
huyo alisema kifo cha Mariam ambaye alifanikiwa kujiokoa, kilisababishwa na
kukosa huduma ya haraka baada ya kuvunjika mguu.
Kamanda
huyo alisema wafanyabiashara hao walivamiwa na majambazi waliokuwa na risasi
pamoja na mapanga katika vibanda vya kubadilishia fedha nchini humo. “Miili ya wafanyabiashara hao ililetwa na ndugu zao ambao
wanaishi Msumbiji,” alisema.
Wakizungumzia
tukio hilo, Said Mfanga na Dotto Ramadhani ambao ni ndugu wa marehemu hao
walisema baada ya kuwaua, majambazi hao waliwapora fedha pamoja na mabegi yao.
No comments:
Post a Comment