AZAM FC imeshindwa kuiengua kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara Simba SC, baada ya jioni ya leo kufungwa bao 1-0 na Coastal Union
Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Shukrani
zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee, ambalo linavunja rekodi ya Azam FC
kutofungwa msimu huu, beki wa kulia Miraj Adam aliyetikisa nyavu za timu ya Azama
kukanako dakika ya 67 ya mchezo.
Kipa Aishi Manula(PICHANI) ana kila sababu ya kubeba lawama kwa bao hilo, kwani alidaka mpira na kulala nao kwa muda mrefu huku akiugulia maumivu badala ya kuutoa nje kwanza na refa Vincent Mlabu kutoka Morogoro aliyesaidiwa na Gasper Ketto na Mohammed Mkono akawaadhibu Azam.
Matokeo hayo yanaifanya Coastal Union ifikishe pointi 16 baada ya kucheza mechi 19 na kupanda hadi nafasi ya 13, kutoka ya 16 ilipokuwa inashikilia mkia, wakati Azam FC inabaki na pointi zake 42 za mechi 17, nyuma ya Yanga SC yenye pointi 43 za mechi 18 na Simba SC pointi 45 za mechi 19.
Kikosi cha Coastal Union kilikuwa
1.
Fikirini Bakari,
2.
Hamad Juma,
3.
Adeyum Saleh Ahmed,
4.
Mbwana Hamisi ‘Kibacha’,
5.
Miraj Adam,
6.
Sabo Youssouf,
7.
Juma Mahadhi,
8.
Abdulhalim Humud,
9.
Abasarim Chidiebere,
10.
Ally Ahmed ‘Shiboli’/Ayoub Yahya
dk78
11.
Nassor Kapama.
Azam FC
1.
Aishi Manula,
2.
Shomary Kapombe,
3.
Erasto Nyoni,
4.
Said Mourad,
5.
Serge Wawa,
6.
Farid Malik/Gardiel Michael dk46,
7.
Michael Balou,
8.
Frank Domayo/Salum Abubakar dk46,
9.
Jean Mugiraneza,
10.
John Bocco
11.
Allan Wanga/Kipre Tchetche dk69.
Mechi Za Leo 2016-02-14
Ft
|
Mwadui Fc
|
0
|
:
|
0
|
T.Prisons
|
Ft
|
Coastal Union
|
1
|
:
|
0
|
Azam Fc
|
Michezo Inayokuja
Jumamaosi 2016-02-20
Jumamaosi 2016-02-20
16:00
|
Yanga
|
Vs
|
Simba Sc
|
16:00
|
Mgambo Jkt
|
Vs
|
T.Prisons
|
16:00
|
Stand United
|
Vs
|
Jkt Ruvu
|
16:00
|
Mbeya City
|
Vs
|
Azam Fc
|
16:00
|
Majimaji
|
Vs
|
Mtibwa Sugar
|
16:00
|
Toto Africans
|
Vs
|
Kagera Sugar
|
Jumapili Februari 21
Ndanda
FC v African Sports
Mwadui
FC v Coastal Union
No comments:
Post a Comment