Ligi Kuu ya Vodacom inatarajiwa kuendelea wikiendi hii mzunguko wa 20 kwa michezo nane kuchezwa katika viwanja mbalimbali huku Jumamosi michezo mitano ikichezwa kwa kila timu kusaka pointi tatu muhimu katika ligi hiyo.
Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Yanga SC v Simba SC watakua wakichuana kusaka uongozi wa Ligi hiyo katika mchezo namba 153, huku Mgambo Shooting wakiwakaribisha Tanzania Prisons katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Wagonga Nyundo wa jiji la Mbeya, Mbeya City watawakaribisha Azam FC katika uwanja wa Sokoine mjini humi, mjini Shinyanga chama la wana Stand United watawakaribisha JKT Ruvu katika uwanja wa Kambarage, huku Toto Africans wakicheza dhidi ya Kagera Sugar katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Jumapili Ndanda FC watakua wenyeji wa African Sports uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, Mwadui FC watakua wenyeji wa Coastal Union uwanja wa Mwadui Complex mkoani Shinyanga, huku wana lizombe Majimaji FC wakicheza dhidi ya Mtibwa Sugar katika uwanja wa Majimaji mjini Songea.
WASEMAVYO
MAKOCHA WA SIMBA NA YANGA, KABLA YA
MCHEZO WA KESHO.
Kocha
wa Simba, Jackson Manyanga, amesema itafanya vizuri dhidi ya Yanga katika mechi
ya keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa kutokana na kuimarika kwa kikosi chake.
Timu hizo zitachuana katika mechi hiyo ya pili ya watani wa jadi msimu huu itakayochezeshwa na refa mwanamama Jonesia Rukyaa kutoka Kagera.
Timu hizo zitachuana katika mechi hiyo ya pili ya watani wa jadi msimu huu itakayochezeshwa na refa mwanamama Jonesia Rukyaa kutoka Kagera.
Alisema timu yake haitarajii kitu kingine zaidi ya ushindi katika mechi ambayo ndiyo itatoa dira ya timu itakayotwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu.
“Wachezaji wetu wako tayari kwa mechi ya watani, Yanga ni timu nzuri yenye wachezaji wazuri na wenye uzoefu na kucheza dhidi yao mara zote ni mechi ngumu, lakini tuko tayari kuwakabili wikendi hii,” alisema.

Mwambusi, kocha wa zamani wa Mbeya City FC, alisema anajua mechi itakuwa mgumu kutokana na ubora wa kikosi cha Simba ambacho kimeshinda mechi zote saba zilizopita za VPL(sita chini ya Mayanja).
“Tunakijua kile ambacho kinawapa matumaini ya kushinda mchezo wa Jumamosi, lakini tumejipanga kuepukana nacho na kushinda kama ilivyokuwa mzunguko wa kwanza. Tutaonyesha ubora wetu siku hiyo uwanjani,” alisema Mwambusi.
Takwimu za Nipashe zinaonyesha kuwa katika mechi 12 zilizopita za watani wa jadi Ligi Kuu tangu mwaka 2010, Simba inayoongoza msimamo wa VPL kwa sasa ikiwa na mtaji wa pointi 45, imefunga mabao 15 dhidi ya Yanga, lakini Wanajangwani wameshinda mara nne huku wapinzani wao wakiibuka na ushindi mara tatu.
Ushindani mwingine mkali unaosubiriwa Jumamosi utawahusisha kinara wa Hamis Kiiza wa Simba na Amissi Tambwe wa Yanga wanaowania kiti cha Simon Msuva cha Mfungaji Bora wa msimu.
Kiiza ametupia mara 16 katika mechi 19ambazo
Orodha
ya Wafungaji Bora
Rn
|
Player
Name
|
Timu
|
Goal
|
1
|
Hamisi Kiiza
|
Simba SC
|
16
|
2
|
Amisi Tambwe
|
Yanga SC
|
14
|
3
|
Donald Ngoma
|
Yanga SC
|
10
|
4
|
Jerema Juma
|
T.Prisons
|
10
|
5
|
Elias Maguli
|
Stand United
|
9
|
6
|
Ibrahim Ajibu
|
Simba SC
|
8
|
7
|
Kipre Tcheche
|
Azam FC
|
8
|
8
|
Shomari Kapombe
|
Azam FC
|
7
|
9
|
Atupele Green
|
Ndanda FC
|
6
|
10
|
John Bocco
|
Azam FC
|
6
|
11
|
Saimon Msuva
|
Yanga SC
|
6
|
12
|
Edward Christopher
|
Toto Africans
|
5
|
13
|
Fully Zully Maganga
|
Mgambo JKT
|
5
|
Rn
|
Timu
|
P
|
W
|
D
|
L
|
F
|
A
|
Gd
|
Pts
|
1
|
Simba Sc
|
19
|
14
|
3
|
2
|
35
|
11
|
24
|
45
|
2
|
Yanga
|
18
|
13
|
4
|
1
|
42
|
9
|
33
|
43
|
3
|
Azam Fc
|
17
|
13
|
3
|
1
|
31
|
11
|
20
|
42
|
4
|
Mtibwa Sugar
|
18
|
9
|
6
|
3
|
21
|
12
|
9
|
33
|
5
|
T. Prisons
|
18
|
8
|
6
|
4
|
18
|
17
|
1
|
30
|
6
|
Mwadui Fc
|
19
|
8
|
5
|
6
|
19
|
16
|
3
|
29
|
7
|
Stand United
|
18
|
9
|
2
|
7
|
18
|
15
|
3
|
29
|
8
|
Mbeya City
|
19
|
5
|
6
|
8
|
20
|
23
|
-3
|
21
|
9
|
Toto Africans
|
19
|
5
|
6
|
8
|
18
|
27
|
-9
|
21
|
10
|
Ndanda Fc
|
19
|
4
|
8
|
7
|
17
|
19
|
-2
|
20
|
11
|
Mgambo Shooting
|
19
|
4
|
5
|
10
|
15
|
24
|
-9
|
17
|
12
|
Coastal Union
|
19
|
3
|
7
|
9
|
13
|
20
|
-7
|
16
|
13
|
Kagera Sugar
|
19
|
4
|
4
|
11
|
10
|
22
|
-12
|
16
|
14
|
African Sport
|
19
|
4
|
4
|
11
|
6
|
19
|
-13
|
16
|
15
|
Majimaji Fc
|
19
|
4
|
4
|
11
|
11
|
32
|
-21
|
16
|
16
|
Jkt Ruvu
|
19
|
3
|
5
|
11
|
18
|
30
|
-12
|
14
|
No comments:
Post a Comment