MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan ameagiza uongozi wa
Halmashauri ya Jiji la Tanga kumaliza haraka mgogoro wa uongozi ndani ya
halmashauri hiyo, kuharakisha utekelezaji wa shughuli za maendeleo kwa
wananchi.
Alitoa agizo hilo katika Ikulu ndogo
ya Tanga wakati akizungumza na viongozi baada ya kupokea taarifa ya maendeleo
ya mkoa wa Tanga baada ya kuwasili kwa ajili ya ufunguzi wa mkutano wa
kimataifa wa mazingira unaoratibiwa na Unesco.
Alisema kwa kuwa uchaguzi mkuu
umekwisha salama, ajenda inayopaswa kutekelezwa sasa ni utekelezaji wa Ilani ya
Chama Cha Mapinduzi kuwezesha wananchi kupata maendeleo.
Alisema serikali ina mpango mkubwa
wa kuwekeza katika viwanda kwenye jiji la Tanga. Hata hivyo alisema endapo
hakutakuwa na uongozi wa Baraza la Madiwani katika halmashauri hiyo, malengo
hayo hayataweza kutekelezwa.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Tanga,
Mwantumu Mahiza akisoma taarifa, alisema mkoa umejipanga na kuweka mikakati ya
kutekeleza mipango mbalimbali katika sekta za elimu, afya, maji, viwanda na
mazingira kuwezesha wananchi kujipatia maendeleo.
![]() |
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi wa Mkoa wa Tanga baada ya kupokea Taarifa ya Mkoa huo kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Mwantumu Mahiza (aliyeketi kulia). |
No comments:
Post a Comment