POLISI
mkoani Tanga imesema imegundua mbinu mpya ya usafirishaji wa dawa za kulevya
aina ya mirungi kwa kuziweka kwenye madumu tupu yaliyokuwa na mafuta.
Mbinu hiyo inadaiwa kutumiwa na
baadhi ya wasafirishaji wa dawa hizo kuziingiza mkoani humo wakikwepa kukamatwa
na askari kwenye vizuizi barabarani.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga,
Mihayo Msikhela aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kwamba
wasafirishaji hao hujaza mirungi ndani ya madumu matupu ya ujazo wa lita 20
yaliyokuwa na mafuta ya kupikia na kisha kuyasafirisha katika magari mbalimbali
ya mizigo.
Alisema wamebaini mbinu hiyo
kutokana na jitihada za askari waliokuwa doria katika kizuizi cha polisi
kilichopo eneo la Amboni kati ya saa 10 hadi 11 jioni baada ya kukamata lori
namba T 342 CVY aina ya Nissan lililokuwa likisafirisha mchanga kwa ajili ya
ujenzi kutoka kijiji cha Mpirani kwenda jijini Tanga.
“Jana jioni askari waliokuwa doria
nje ya mji eneo la Mpirani lililopo kata ya Chongoleani walikamata watu saba
waliokuwa wakisafirisha kilo 73 za mirungi kwa kutumia lori la mchanga kwa
kuweka dawa hizo ndani ya madumu yaliyokuwa yametumika kuhifadhia mafuta ya
kula na kisha kuyafunika na kifusi cha mchanga kilichokuwa ndani ya lori hilo”,
alisema.
Aliongeza, “Baada ya kujaza mirungi
madumu hayo waliyafukia ndani ya shehena ya mchanga uliokuwa unasafirishwa
kwenda eneo la Kwanjeka jijini Tanga kuuzwa kwa mteja”, alisema.
Kamanda Mihayo aliwataja watuhumiwa
wanane waliokuwa wakisafirisha mirungi hiyo ambao wote ni wakazi wa mkoani
hapa, akiwemo dereva wa lori.
Alisema wote watafikishwa
mahakamani.
Kamanda wa
Polisi Tanga, Mihayo Msikhella akiwaonyesha waandishi wa habari miongoni mwa
sukari iliyokamatwa katika bandari bubu ya Kigombe Pangani wakati wa doria
iliyofanyika kwa siku mbili mfululizo na kufanikiwa kukamata mifuko 81 ya
sukari inayotoka Pakistan, Indonesia na India.
|
No comments:
Post a Comment