HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 2 April 2015

WAKAZI WA KISIWA CHA FUNDO HUKO PEMBA WAONJA JOTO YA JIWE KWA KUKUBALI SERA ZA SERIKALI KUHUSU UTALII.



Na Masanja Mabula -Pemba
Wakaazi wa Kisiwa cha Fundo wanaokubaliana na sera za Serikali ya kuimarisha uchumi wake kupitia sekta ya Utalii waanza kuonja machungu ya kususiwa pamoja na kutopewa huduma za kijamii ikiwemo za mahitaji ya kila siku za nyumbani .
Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba
Mhe Omar Khamis Othman
Tayari wananchi hao wamekuwa na wakati mgumu kutokana na kukosa huduma ya chakula madukani pamoja na huduma za usafiri wa kutoka Kisiwani humo kwenda Wete .

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi baadhi ya wananchi ambao wameonja joto ya kususiwa wameiomba serikali ichukua hatua za haraka za kukumaliza mgomo huo ili waweze kuendelesha maisha yao bila ya hofu .

Wamesema kuwa baadhi ya wananchi tayari wamewahi kushushwa katika vyombo vya baharini licha ya kwamba walikuwa na mizigo na watoto wachanga .

"Mimi nilishushwa kwenye mashuwa nikiwa na mtoto mchanga pamoja na mizigo nikiwa maji ya shingoni , nilijikokota na kwa bahati ilikuja boti ya mwekezaji kunichukua baada ya kupewa taarifa na wasamiria wema " alieleza mmoja wa wahanga hao .

Aidha wapo baadhi yao ambao wamepata adha ya kutomeshwa na mbwa na na vijana jambo ambalo linaweza kusababisha kuwepo na uvunjfu wa amani kwa wakaazi wa Kisiwa hicho .

Akizungumzia hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman ametakiwa wafanyabishara hao kuendesha biashara zao kwa mujibu wa sharia na leseni zao kwa kuhakikisha kwamba wanatoahuduma kwa wananchi wote bila ya ubaguzi Amesema kuwa Serikali ya Mkoa haiwezi kukaa kimiya wakati wananchi wake wanaendelea kuteseka kwa kukosa kupatiwa huduma na mahitaji muhimu ya kijamii .

"Serikali haiweze kuvumilia matendo ya aina hii kuendelea kutokea , ni vyema wafanyabiashara kufuata sheria ambazo zimo katika mikataba ya biashara yao kwa kuhakikisha wanatoa huduma kwa wote bila ya ubaguzi " alisema .
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amesema iwapo wafanyabiashara hao wataendelea kukaidi agizo hilo , hatua za kisheria zitachukuliwa na taasisi husika ikiwa ni pamoja na kupokonywa leseni za biashara zao .

"Iwapo wataendelea na mgomo huo basi hatua za kuwapokonywa leseni za biashara zao zitachukuwa na vile vyombo vya baharini vitapandishwa juu na serikali itaweka chombo kwa ajili ya wananchi wote wa Fundo " alifahamisha .

Mgomo huo umekuja kufuatia Serikali kuruhusu mwekezaji kuwekeza katika Kisiwa hicho huku baadhi ya wakaazi wake wakiwa wanapinga kuwepo na mwekezaji katika Kisiwa hicho .

No comments:

Post a Comment