HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 2 April 2015

MKUU WA MKOA WA KASKAZINI PEMBA ATAKA WANACHI WASHIRIKISHWE KWENYE UPIMAJI WA ARDHI.

Na Masanja Mabula. PEMBA

Mkuu wa mkoa wa kaskazini Pemba mhe omar khamis Othman amewataka watendaji wa Idara ya Upimaji Pemba kuwashirikisha wananchi wakati wa upimaji wa ardhi ili kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima .

Amesema kuwa migogoro mingi ya ardhi inayotokea katika mkoa huo inasababishwa na watendaji wa Idara ya Upimaji kutowashirikisha wananchi wakati wa upimaji .

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba
Mhe Omar Khamis Othman
Kauli hiyo ameitoa huko ofisini kwake wete wakati akizungumza na watendaji wa Idara ya Upimaji Pemba , Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Micheweni katika kikao cha kusuluhisha mgogoro wa ardhi iliyoko Makangale kati ya Mzee Ali Said na mwakilishi wa Mhe Samiya Suluhu Hassan .

Aidha mkuu huyo wa Mkoa amefahamisha kwamba wananchi wanaozitumia ardhi hizo wanapaswa kushirikishwa wakati wa upmaji kwa kulipwa fidia ya vipando na  mazao  yao yaliyomo katika maeneo yanayopimwa .
Naye katibu Tawala Wilaya ya micheweni Bw Hemed Khalid Abdalla ameitaka Idara ya Upimaji Pemba kusaidia kupunguza migogoro ya ardhi kwa kuhakikisha kwamba wanafuata misingi ya utawala bora ya ushirikishwaji .

Amesema kuwa migogoro ya ardhi ambayo inajitokezwa katika Wilaya ya Micheweni inaweza kuzuiwa iwapo Idara ya Upimaji itawashirikishwa wnanchi wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kazi zake .

No comments:

Post a Comment