HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 2 April 2015

VIJANA WA SOBER HOUSE PEMBA WAIOMBA SERIKALI KUWAPATIA DAWA ZA KUTIBU MAJI.


Vijana wanaoishi kwenye nyumba za kurekebisha tabia (SOBA HOUSE) iliyoko Pemba

Na Masanja Mabula .PEMBA
Vijana wanaoishi kwenye nyumba za kurekebisha tabia (SOBER HOUSE)baada ya kuamua kuachana na utumiaji wa  dawa za kulevya  Wilaya ya wete pemba wameiomba Serikali kuwapatia dawa za kinga  ya maji ili kuwanusuru kupata maradhi ya mripuko .
Mratibu wa nyumba hizo abdulwahid salim said amesema kuwa kutokana na mvua za masika ambazo zinaendelea kunyesha kwa sasa uwezekano wa kupata maradhi ya mripuko ni mkubwa iwapo hakutachukuliwa hatua za haraka .
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko katika nyumba namba moja iliyoko Limbani , amesema kuwa kwa sasa baadhi ya vijana wamekuwa wakabililiwa na matumbo ya kuharisha  yanayotokana na kunywa maji ambayo hayako salama kwa afya za wananchi  .

Amesema kuwa pamoja na kwamba wanatumia maji ya bomba  lakini yanahitaji kuchemshwa kabla ya kutumika jambo ambalo linawawia vigumu kutokana na gharama kubwa hivyo wameomba kupatiwa wate guard ili waweze kunusuru kupata maradhi ya mripuko .

"Katika kipindi hichi ambapo mvua  za masika zinaendelea kunyesha uwezekano wa kupata maradhi ya mripuko ni mkubwa , hivyo tunaomba kupatiwa dawa ya maji ili kuweza kunusuru afya zetu " alieleza .

Aidha abdulwahid ameeleza kwamba mbali na kukabiliwa na changamoto hiyo lakini vijana wanaoishi katika nyumba hizo wanaweza kupata maaedhi ya kuambukiza kutokana na mgodoro wanayotumia kuwa ni muda mrefu .
Amesema kuwa magodoro hayo yanaendelea kutumika tangu miaka mitatu iliyopita ambapo vijana wanaoingia na kutoka wanayatumia bila ya kujua athari zinazopweza kuwapata .

"Magodoro yaliyopo ni ya zamani na vijana wanaiongia na kutoka kila siku , pia tunahofu kwamba kunaweza kutokea maradhi ya kuambukiza kutokana na magodoro yanayotumika na vijana " alifahamisha . 
Kutokana na changamoto hiyo ametupa lawama kwa Viongozi wa majimbo Wabunge na Wawakilishi kwa kushindwa kuzitembelea nyumba hizo na kuwashukuru Viongozi wakuu wa Nchi kwa kuwa na utaratibu wa kuwatembelea mara kwa mara .

"Tunatambua uwepo wa viongozi wa majimbo Mbunge na Mwakilishi , lakini sisi hatujawaona kututembelea ambapo viongozi wakuu wa nchi wamekuwa na kawaida ya kututembelea lakini viongoji wa majimbo hatuwaoni " alisema .
 Wilaya ya Wete ina nyumba mbili ambazo zinatoa programu kwa vijana wanaoacha matumizi ya dawa za kulevya ambapo jumla ya 53 kutoka Bara na Visiwani wanaendelea na programu zao katika nyumba hizo .

No comments:

Post a Comment