HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 9 April 2015

SERIKALI YA SANZIBAR YATAKIWA KUTOA ELIMU YA UJASIRIAMALI KWA VIJANA WA PEMBA.



Na Masanja Mabula.PEMBA
Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya mkipi miliki Bw Mohammed Abdalla Foum amesema  elimu ya  ujasiriamali inahitaji kutolewa ili kuwawezesha vijana kujiajiri wenyewe kupitia dhana ya kujitegemea .

Amesema kuwa serikali imeweka fursa nyingi ambazo zinaweza kusaidia vijana kuondokana na umaskini pamoja na matendo maovu ikiwemo ya utumiaji wa madawa ya kulevya .

Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi  ambapo pia amesisitiza haja kwa vijana kubuni miradi ambayo  itakuwa ni mkombozi kwao na familia zao .

Naye msaidizi afisa uendeshaji wa kampuni hiyo Mwalimu  Omar Khamis ali amezishauri taasisi zinazotoa mikopo , kutoa kipaombele kwa vijana ambao wamejikusanya pamoja kwa lengo la  kupambana na umaskini wa kipato .
Hivyo amewataka vijana kuondoa dhana ya kutegemea ajira kutoka serikalini , bali wajikusanye pamoja na  kuanzisha mikundi vya uzalishaji mali .

No comments:

Post a Comment