HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 25 March 2015

YANGA YAPETA LIGI KUU TZ BARA "MSUVA AMPOROMOSHA KAVUMBAGU KWENYE UFUNGAJI"




Kiungo hatari
Simon Happygod Msuva(kulia)
Ligi kuu ya Soka Tanzania Bara imeendelea jana kwa mchezo mmoja wa kiporo kati ya Yanga na JTK Ruvu katika Dimba la Taifa jijini DSM, mchezo uliomalizika kwa Yanga kushinda bao 3-1 na kupaa point 4 mbele ya timu ya pili kwenye msimamo wa ligi timu ya Azam Fc.
  
Katika mchezo huo mabao ya yanga yamefungwa na Simon Msuva baada ya shuti kali alilopiga kushikwa na Amosi Makwaya  na refarii kutoa adhabu ya Penalt iliyofungwa na Msuva mwenyewe dakika ya 35. Bao la pili limefungwa kufuatia krosi ya winga hatari simon Msuva kumkuta Danny Mrwanda anayefunga na kuiandikia Yanga goli la pili dakika ya 42.
Bao la tatu limepatikana kipindi cha pili likiwekwa kimiani na Simon Msuva tena dakika ya 57.
Bao la kufutia machozi kwa upande wa JKT Ruvu lilifungwa na Samuel kamuntu mwishoni mwa kipindi cha kwanza cha mchezo huo.
Kiungo Simon Happygod Msuva amefikisha mabao 11 na kumpita aliyekuwa kinara wa ufungaji mshambuliaji wa Azam Didier Kavumbagu mwenye magoli 10.

Kavumbagu raia wa Burundi amekuwa akiongoza kwa ufungaji tokea kuanza kwa ligi hiyo.

MSIMAMO WA LIGI KUU

Rn
Timu
P
W
D
L
F
A
Gd
Pts
1
YANGA
19
12
4
3
28
11
17
40
2
Azam FC
18
10
6
2
25
12
13
36
3
SIMBA SC
20
8
8
4
25
14
11
32
4
KAGERA SUGAR
19
6
7
6
16
17
-1
25
5
Coastal Union
20
5
9
6
14
14
0
24
6
JKT RUVU
20
6
6
8
16
19
-3
24
7
MGAMBO
19
7
3
9
13
19
-6
24
8
MTIBWA SUGAR
18
5
8
5
18
18
0
23
9
MBEYA CITY
19
5
8
6
14
16
-2
23
10
RUVU SHOOTING
20
5
8
7
13
18
-5
23
11
NDANDA FC
20
6
5
9
17
23
-6
23
12
POLISI MORO
20
4
9
7
13
17
-4
21
13
STAND UNITED
19
5
6
8
16
23
-7
21
14
T. PRISONS
19
2
11
6
13
20
-7
17
LIGI KUU VODACOM
RATIBA
Jumamosi Aprili 4
Mtibwa Sugar v Stand United
Coastal Union v Tanzania Prisons
Ruvu Shooting v Ruvu JKT
Ndanda FC v Mbeya City 
Kagera Sugar v Simba (Mechi kuchezwa Kambarage, Shinyanga)

No comments:

Post a Comment