HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 25 March 2015

MKUU WA MKOA WA TANGA AVITAKA VITUO VYA AFYA KUTUMIA FURSA YA MIKOPO ITOLEWAYO NHIF.



MKUU wa Mkoa wa Tanga, Said Magalula, amevitaka vituo vya afya mkoani hapa kutumia fursa ya mikopo itolewayo  na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) ikiwemo vifaa tiba na madawa  na kuweza kuwa msaada kwa wananchi katika kupata huduma zilizo  bora.

Akizungumza katika kikao cha uhamasishaji mpango wa mikopo ya vifaa tiba  kilichofanyika hospitali ya Mkoa ya Bombo, Magalula amewaagiza waganga wakuu wa hospitali Mkoani na Wilayani kuitumia nafasi hiyo itolewayo na Bima ya Afya.
Amesema kelele za wananchi kulalamikia huduma mbovu zitolewazo katika vituo  imezidi wakati ziko fursa za kupunguza kero hizo kwa kukopa vifaa pamoja na ukarabati wa majengo jambo ambalo ni nadra kuipata nafasi hii tuitumie vizuri.
Magalula amesema ni muhimu kuzichangamkia  fursa hizi ili kupunguza kelele za wananchi kulalamikia huduma mbovu zikiwemo uhaba wa madawa na vifaa katika hospitali zetu
Mkuu wa mkoa ametoa agizo kwa waganga wakuu wa hospitali zote za mjini na Wilayani kuhakikisha wanaitumia ipasavyo fursa hii na kumaliza manung’uniko kutoka kwa wananchi juu ya hospitali na vituo vyetu vya afya.
Pia amesema baadhi ya vituo vya afya majengo yake yako katika mazingira hatarishi na mengine kufikia hatua ya  kutaka kuanguka na hivyo kuwaagiza kuchangamkia nafasi inayotolewa na mfuko wa bima ya afya ili kuyanusuru  majengo mengi yako katika hali mbaya ikiwemo miundombinu ya kupitishia maji ni uchakavu wa majengo jambo ambalo linaondoa taswira ya mazingira ya afya kwa wananchi.
Kwa upande wake Meneja wa Taifa Mfuko wa Bima ya Afya Mkoa wa hapa , Ali Mwakababu, amesema mbali ya elimu na matangazo mengi lakini hadi sasa ni vituo vichache ambavyo vimejitokeza kutaka mikopo.
Mwakababu amesema elimu bado inahitajika na hivyo kuitaka Wizara ya Afya Mkoa kutoa elimu kwa Waganga wakuu wa Wilaya kuomba mikopo ambayo inaweza kusaidia kuimarisha huduma zao zikiwemo matibabu na ukarabati wa majengo.
Meneja amesema mwaka 2007 Bima ya Afya ilianzisha huduma ya kutoa mikopo ni vituo vichache ambavyo vimeomba mikopo ya kukarabati majengo kwani majengo mengi ni chakavu na hayana vifaa tiba mfano madawa ,na Ex ray amesema pia wanatoa.
Hata hivyo Meneja amewataka waganga wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanamaliza changamoto wanazokabiliana nazo katika vituo vyao  lengo likiwa ni kuboresha huduma  kwa wananchi.

No comments:

Post a Comment