HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 24 March 2015

SHEHA ASIMAMISHWA KAZI KWA TUHUMA ZA KUM'BAKA MWANAE WA KUUMZAA HUKO PEMBA.



Na Masanja Mabula aliyeko Mkoa wa kaskazini -pemba.
Sheha wa shehia ya majenzi wilaya ya micheweni mkoa wa kaskazini  pemba Bw Omar Pandu Kai amesimamishwa kazi na mwajiri wake kutokana na tuhuma za kumbaka mwanawe wa kumzaa  wa kike anayekisiwa kuwa na umri wa miaka 14.

Kwa mujibu wa taarifa ya mkuu wa mkoa wa kaskazini pemba mhe omar khamis othman ni kuwa uwamuzi wa kumusimamisha kazi sheha hiyo zimekuja baada ya kupata taarifa kutoka kwa vyombo vya usalama vya mkoa huo .

Amesema kuwa sheha huyo amekiuka maadili ya uongozi na kwamba amesimamishwa ili kupisha vyombo vya ulinzi viweze kufanya kazi yake na kuvitaka kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria .

Mkuu huyo wa mkoa amesema hatakuwa tayari kuona kuwa kiongozi wa serikali ambaye ataonekana kwenda akinyume na taratibu za uongozi na kwamba atamwajibisha kwa mujibu wa sheria za utumishi wa umma .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi sheha wa shehia mtemani wete juma mrisho magogo amesema kuwa kitendo kilichofanywa na sheha huyo kimeshusha hadhi ya kazi yao .

Sheha magogo amesema kuwa ni vyema vyombo vya sheria kufanya uchunguzi wake na kisha vichukuwe hatua kwa mujibu wa sheria za nchi ili kudhibiti matendo ya udhalilishaji .

No comments:

Post a Comment