![]() |
| Silaha iliokamatwa kwenye tukio la Amboni. |
Watu 10 wakazi wa jiji la Tanga wamefikishwa tena
kwa mara ya pili mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga wakikabiliwa na kesi
ya kuhusishwa na makosa matano tofauti kuhusiana na tukio la kuwanyang’anya
Polisi SMG mbili zenye risasi 60 pamoja na kuua Askari wa Jeshi la Wananchi
Tanzania (JWTZ) Sajenti Mohamed Kajembe.
Wahusika ni Mbega Seif (25)
maarufu ‘Abuu Rajab, ambaye ni Mfanyabiashara mkazi wa Kiomoni, Rajabu Bakari
(19) mwanafunzi mkazi wa Makorora, Ayubu Ramadhani (27) maarufu ‘Chiti’ ambaye
ni Fundi umeme na mkazi wa Kona Z Kiomoni, Hassani Mbogo (20) maarufu
Mpalestina ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Makorora, Mohamed
Ramadhani (19)Mfanyabiashara na mkazi wa Makorora, Sadiki Mdoe (25)almaarufu
kama kizota mkazi wa Magaoni.
Wengine ni Saidi Omari (26)mfanyabiashara na mkazi wa Magaoni tairi tatu, Nurdin Mbogo (27) Makorora, Ramadhan Mohamed (18)mfanyabiashara na mkazi wa Donge pamoja na Omari Abdala (55) maarufu ‘Ami’ mkazi wa Makorora Dunia Hoteli.
Wengine ni Saidi Omari (26)mfanyabiashara na mkazi wa Magaoni tairi tatu, Nurdin Mbogo (27) Makorora, Ramadhan Mohamed (18)mfanyabiashara na mkazi wa Donge pamoja na Omari Abdala (55) maarufu ‘Ami’ mkazi wa Makorora Dunia Hoteli.
Walifikishwa mahakamani majira
ya saa tatu za asubuhi wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ambapo ulinzi
uliendelea kuimarishwa ndani na nje ya mahakama hiyo wakati shauri hilo
likiendelea mahakamani.
Akizungumza mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Aziza Rutala Wakili wa serikali MariaClara Mtengule,alimwomba Hakimu kusogeza mbele kesi hiyo kutokana na upelelezi wa baadhi ya makosa yanayowakabili watuhumiwa hao kutokamilika.
Akizungumza mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Aziza Rutala Wakili wa serikali MariaClara Mtengule,alimwomba Hakimu kusogeza mbele kesi hiyo kutokana na upelelezi wa baadhi ya makosa yanayowakabili watuhumiwa hao kutokamilika.
Hata hivyo Rutala alikubaliana
na ombi hilo na kusema kuwa kesi hiyo itatajwa tena Aprili 8, mwaka huu na
kwamba washtakiwa wote wanatakiwa kwenda rumande kutokana na makosa
yanayowakabili kutokuwa na dhamana.
Katika kesi la awali
inayowakabili wakazi hao wa Jiji la Tanga, kosa la kwanza hadi la tatu
linawahusisha washatakiwa namba moja mpaka nane kwa kuhusika kula njama ya
kutenda kosa kinyume cha sheria ya kanuni ya adhabu namba 384 sura ya
16 ya mwaka 2002.
Katika kosa la pili linadaiwa
kutendeka mnamo Januari 26 mwaka huu katika mgahawa wa Jamali ulipo kati ya
barabara ya nne naya tano jijini Tanga washitakiwa wote nane waliiba silaha moja
aina ya SMG namba za usajili 14303545 mali ya Jeshi la Polisi Tanzania na
muda mfupi kabla ya kutenda kosa hilo walitumia visu kumchoma askari H 501
Mwalimu ili kupata silaha hiyo.
Ilielezwa kuwa kosa la
tatu la unyang’anyi wa kutumia silaha washtakiwa wote nane katika mgahawa
wa Jamali uliopo kati ya barabara ya nne naya tano waliiba silaha nyingine
yenye namba za usajili 14301230 SMG mali ya Jeshi la polisi Tanzania na kwamba
muda mfupi kabla ya kutenda kosa hilo walimtishia kwa kutumia nguvu
kumnyang’anya silaha askari polisi H Mansoor kinyume na sheria namba 287(a) ya
kanuni ya adhabu kifungu 16 ya mwaka 2002.
Katika kosa la nne ambalo
limemuhusisha mshatakiwa namba tisa Nurdin Mbogo wakili wa serikali Barasa
alisema mnamo Februari 6 mwaka huu katika sehemu isyofahamika jijini Tanga
mshtakiwa huyo akijua kuwa Hassan Mboko (Mshatakiwa Na. 4) alitenda kosa
Septemba mosi 2014 na Januari 26 mwaka huu alimsaidia kumwezesha kukwepa
kushtakiwa na kuadhibiwa kinyume na sheria namba 387 (I) na sheria namba 384 ya
2002.
Shtaka la tano liliwahusisha washtakiwa namba moja,mbili na namba 10 kwa kuhusika kumuua Askari wa JWTZ Sajenti Mohamed Rashid Kajembe mnamo Februari 13 mwaka huu katika Mapango ya Amboni Jijini Tanga kinyume cha sheria namba 196 na 197 ya makosa ya adhabu ya mwaka 2002 .
Shtaka la tano liliwahusisha washtakiwa namba moja,mbili na namba 10 kwa kuhusika kumuua Askari wa JWTZ Sajenti Mohamed Rashid Kajembe mnamo Februari 13 mwaka huu katika Mapango ya Amboni Jijini Tanga kinyume cha sheria namba 196 na 197 ya makosa ya adhabu ya mwaka 2002 .
Washtakiwa hao hawakutakiwa
kujibu lolote kutokana na Mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi
hiyo ya mauaji.
Hii ni mara ya pili kw
watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani hapo ambapo kwa mara ya kwanza walisomewa
mashitaka yao Machi 9 mwaka huu.

No comments:
Post a Comment