HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 23 March 2015

AJALI ZA BARABARI ZAUA WATATU TANGA.


Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani R.T.O Abdi Isango akizungumza na baadhi ya madereva wa bodaboda jijini Tanga.

WATU watatu wamepoteza maisha katika matukio matatu tofauti yaliyohusisha ajali za barabarani mkoani Tanga.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Juma Ndaki amesema mnamo tarehe 20/03/2015 mtembea kwa miguu asiyefahamika jina  amegongwa na gari ambalo halikutambulika na kufariki papo hapo katika kijiji cha kitumbi  kata ya Kwamkonga wilayani Handeni.

Tukio lingline ni la kijiji cha Mabalaga kata ya Mabalaga barabara ya kuelekea Kwadiboma Wilayani Handeni, gari aina ya fuso lori lenye na T403 AHR lililokuwa linaendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina moja la Abdalah, limepinduka na kusababisha kifo cha mtu mmoja.

Kamanda Ndaki amemtaja marehemu kuwa ni Selemani Rajabu mwenye umri wa miaka 48  mkazi wa Gitu ambae kifo chake kimetokana na  kubanwa na mikungu ya Ndizi ambapo watu wanne wamejeruhiwa,  chanzo cha ajali hiyo ikiwa ni utelezi barabarani uliotokana na mvua zinazo endelea.

Katika barabara ya Tanga–Muheza gari aina ya Toyota Pasho no T.885 CUD likiwa na dereva Salehe Mayanjo alimgonga mwendesha baiskeli Twaha Omary mwenye miaka 75 aliye fariki papo hapo.

Kaimu kamanda Ndaki amesema Jeshi la Polisi linaendelea kuchunguza chanzo cha ajari hiyo ambayo hakijafahamika na dereva anashikiriwa kwa hatua za kisheria.

No comments:

Post a Comment