HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 23 March 2015

WABAGUZI WA RANGI WAMVAA MCHEZAJI EMENIKE WA NIGERIA NCHINI UTURUKI"ASHINDWA KUCHEZA NA KUTOKA UWANJANI"





Mshambuliaji wa Emmanuel Emenike wa Fenerbahce amekuta akishindwa kujizuia na kulazimisha afanyiwe mabadiliko na kutolewa nje hata kabla ya kipindi cha pili.

Katika mechi hiyo ya Ligi kuu ya Uturuki dhidi ya wapinzani wao Besiktas, Emenike raia wa Nigeria alilazimisha kutoka na kuvua jezi wakati mashabiki walipoanza kumshambulia kwa maneno makali yakiwemo ya kibaguzi.
Mashabiki hao walikuwa wakimzoea baada ya kushindwa kutuliza mpira mrefu aliopigiwa.
 
Hali hiyo ilionyesha kumuudhi ingawa mashabiki hao pia walilalama kwamba msimu huu amekuwa hana msaada kwa timu yao.
Pamoja na kufanikiwa kutoka, Emenike alirudishwa na benchi la ufundi akiwemo kocha wa timu hiyo ambaye hata hivyo baadaye alilazimika kumtoa baada ya kipindi cha kwanza kwisha.

Ubaguzi wa rangi umekuwa ukiendelea katika nchi mbalimbali ikiwemo Uturuki ambayo ndiyo nchini pekee duniani iliyo katika mabara mawili ya Asia na Ulaya.

Asilimia kubwa ya Waturuki ni wale wenye asili ya Waarabu, lakini ajabu nao wamekuwa na tabia hizo mbovu za hovyo za ubaguzi wa rangi.

No comments:

Post a Comment