HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 23 March 2015

VIONGOZI WA ETHIOPIA, MISRI NA SUDAN WAPATANA KUHUSU MAJI YA MTO NILE.!



Viongozi wa Ethiopia, Misri na Sudan wamesaini makubaliano ya awali ya kusitisha mgogoro wa muda mrefu unaohusu kugawana maji ya mto Nile na ujenzi wa bwawa kubwa zaidi barani Afrika la kuzalisha umeme. 
Viongozi wa Ethiopia, Misri na Sudan
Viongozi hao walisaini makubaliano hayo jana mjini Khartoum, Sudan.Kwa muda mrefu Misri imekuwa ikipinga ujenzi wa bwawa kuu la Ethiopia la kuzalisha umeme, ikisema bwawa hilo litaleta matatizo ya ukosefu wa maji kwa Misri. 

Mwaka 2013, bunge la Ethiopia liliridhia makubaliano mapya yenye utata ili kuchukua nafasi ya mikataba ya kikoloni ambayo iliipatia Misri na Sudan viwango vikubwa vya maji ya mto Nile. Aliyekuwa rais wa Misri wakati huo Bw Mohammed Morsi alisema hataki vita, lakini hataruhusu upungufu wa maji nchini Misri kuathirika kutokana na bwawa hilo. 

Mrithi wa Bw Morsi, Rais Abdul Fattah al-Sisi jana alisaini makubaliano na Waziri Mkuu wa Ethiopia Halemariam Delasegn na Rais wa Sudan Omar al-Bashir kuhusu kugawana maji ya mto Nile. Viongozi hao watatu wamekaribisha kusainiwa kwa makubaliano hayo katika hotuba walizotoa mjini Khartoum baada ya kusaini.

No comments:

Post a Comment