HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 26 March 2015

WAWILI WAKAMATWA NA BUNDUKI (SMG NA SAR) KATIKA HARAKATI ZA KUTEKELEZA MAUAJI.



POLISI mkoani Katavi imewakamata wakazi wawili wa mkoa wa Mwanza wanaotuhumiwa kukodiwa  kumuua  mkazi wa  mjini Mpanda  wakiwa  na  risasi za sialaha nzito za SMG na SAR   na bunduki aina ya  shotgun na risasi  zake tano  kinyume cha sheria .
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi , Dhahiri Kidavashari  aliwataja watuhumiwa  hao kuwa ni pamoja na Vicenti Yusuph (31) na Mkuki Juma miaka (25)ambao  pia walikutqa na  sare za jeshi .

Kamanda Kidavashari hata  hivyo  hakuwa tayari  kumtaja mkazi  huyo wa mjini Mpanda. Alifafanua  kuwa  tukio hilo lilitokea jana saa tisa na nusu  jioni  katika eneo la Mjimwema mjini Mpanda.

“Kukamatwa  kwa  watuhumiwa hawa  kumewezekana  baada ya kupata  taarifa za siri   kutoka kwa raia wema……. Hivyo  tulitega mtega  na tukafanikiwa kuwanasa a walipohojiwa walikiri  kuwa walikodiwa kumuua mkaziwa mjini Mpanda (jina limehifadhiwa)
Kadhalika walikiri kuwa  walikuja mkoani hapa  ili  kufanya  uhalifu  kwa  kuvamia  maeneo ya minada  na kupora fedha “ alibainisha.
Kwa mujibu  wa Kidavashari  watuhumiwa  hao  wanatarajiwa kufikishwa mahakamani  mara tu baada  ya upelelezi wa awali wa shauri  lao kukamilika.

Katika mkasa mwingine , kwa mujibu wa kamanda Kidavashari  Polisi mkoani humo inamshikilia mkazi  wa kijiji cha Katumba wilayani Mlele ,Hamadi Said miaka (29)  akiwa na  ngozi ya chui  yenye thamani ya zaidi  ya Sh milioni 5.7  ya chui  aliyeuawa.
Kidavashari  alidai kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa jana mchana  katika Mtaa wa Kawajense  alitafuta mnunuzi wa nyara hiyo ya Serikali ambapo atafikishwa mahakamani  mara tu  upelelezi wa awali  wa shauri lake  utakapokamilika .

No comments:

Post a Comment