HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 26 March 2015

MAALIM SEIF ASEMA ZANZIBAR INAUNGA MKONO JUHUDI ZA KUHIMIZA AMANI DUNIANI.



Na Masanja Babula .PEMBA.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amesema Zanzibar inaunga mkono juhudi zinazochukuliwa na taasisi ya Kimataifa ya Global Peace Foundation katika kuhimiza amani na utulivu Duniani.
Maalim Seif
Maalim Seif amesema hayo jana  wakati alipokuwa na mazungumzo na ujumbe kutoka jumuiya hiyo, ulioongozwa na Rais wake, James Flynn huko ofisini kwake Migomnani mjini Zanzibar.

Amesema Dunia inakabiliwa na matukio mengi yanayo hatarisha amani na utulivu, hivyo mchango wa jumuiya hiyo ni muhimu katika kupatikana ufumbuzi wa migogoro hiyo na kuwezesha watu kuishi katika hali ya utulivu na kuvumiliana.
Maalim Seif amesema kwa upande wa Zanzibar kuna kila sababu ya kujivunia mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa watu wake kuishi kwa kuvumiliana, licha ya kuwepo watu wenye imani tafauti za kidini, na itikadi za kisiasa.

Amesema hatua hizo zitawaepushia kuchukua maamuzi yasiyokuwa ya busara yanayosababishwa na vijana kupoteza mweleko wa kimaisha ambapo matokeo yake ni amani na utulivu wa nchi kuvurugika.

Naye Rais wa Jumuiya hiyo, James Flynn amesema nguvu kubwa wanazielekeza kusaidia ujenzi wa familia zinazozingatia maadili mema, pamoja na kushirikiana na Serikali za nchi tafauti kusimamia utawala bora ambao una umuhimu wa kipekee katika kudumishwa amani na utulivu.  

No comments:

Post a Comment