HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 26 March 2015

WANANCHI ZAIDI YA 500 WA KIGOMBE WASHIRIKI ZOEZI LA USAFI PAMOJA NA WAWEKEZAJI NA KUKUSANYA ZAIDI YA TANI MOJA YA TAKA.



Zaidi ya Wanakijiji 500 wa Kijiji cha Kigombe kilichopo kata ya Kigombe Wilayani Muheza mkoani Tanga wakiongozwa na viongozi wao wameshiriki kwenye zoezi la msaragambo wa kusafisha maeneo mabilimbali ya kijiji hicho hasa kwenye fukwe za bahari ya hindi ambapo takataka hutupwa kwa wingi na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho.
Mdau wa Usafi kijijini hapo Bw Athumani Mtoro
(watatu kutoka kushoto) akiwa na wadau wengine
wa usafi namaendeleo kijijini hapo.

Zoezi hili limefanikisha kukusanywa kwa zaidi ya tani moja ya taka huku zaidi ya kg 900 zikikusanywa upande wa fukwe za habari pekee.
Fukwe za Kigombe
Akizungumza na waandishi wa habari mdau wa Usafi kijijini hapo Bw Athumani Mtoro amesema wanawashukuru wawekezaji wa Hoteli ya Peponi Beach Resort ambao ndio walio andaa na kuratibu zoezi hilo kwani limeamsha ari ya wananchi kufanya usafi kwenye maeneo yao na kuacha tabia ya kutupa taka hovyo.

Zoezi hilo lililofanyika March 26 mwaka huu pia limeshirikisha wanafunzi kutoka shule ya Sekondari Kigombe likiwa na kauli mbiu isemayo Usafi ni Afya.

No comments:

Post a Comment