HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 27 March 2015

SHULE 10 ZA SEKONDARI TANGA KUSHIRIKI MBIO ZA KUCHANGISHA FEDHA KWA VITUO VYA KULEA WATOTO YATIMA.



Zaidi ya Wanafunzi 200 kutoka shule 10 za Sekondari jijini Tanga watashiriki kwenye michuano maalum ya Riadha kwa ajili kuchangisha fedha za kusaidia vituo vya kulelea watoto yatima na Wajane vya Chumbageni, Makorora na Mwakizaro jijini hapa.
Mbio hizo zitakuwa za umbali wa km 8 kituo cha kwanza kikiwa ni Shule ya Sekondari Popatlal kupitia barabara ya Raskazoni kwenda barabara ya Tanga Beach kurudi mpaka Shule ya Old Tanga ambapo kutakuwa na kituo cha ukaguzi na kurejea tena Shule ya Sekondari Popatlal kwa barabara ya Bombo kilipo kituo cha mwisho.

Akizungumza na mtandao huu Mratibu wa Mbio hizo Mr Ropert kutoka shule ya Sekondari Popatlal amesema shule kumi zimethibitisha kushiriki huku mashirika binafsi na yauma yakiunga mkono na yakiruhusiwa kushiriki mbio hizo ili kuongeza chachu ya mashindano.

Shule shiriki ni Usagara Sec, Eckenforde Cambridge Sec,Chumbageni Sec, Toledo Sec, Nguvumali Sec, Mnyanjani Sec, Mikanjuni  Sec, Old Tanga Sec,Mkwakwani Sec na Wenyeji Popatlal ambao ndio wameandaa mashindano hayo.

Mshindi wa kwanza atazawadiwa Baiskeli wa pili atapata Redio na watatu atajinyakulia Pea moja ya Viatu vya michezo.

No comments:

Post a Comment