HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 30 March 2015

WATUMISHI WA MUNGU WATAKIWA KUFANYA MAANDALIZI YA KUTOSHA KABLA YA KUHUBIRI NENO LA MUNGU.



WATUMISHI wa Mungu nchini wametakiwa kuhubiri na neno la Mungu wakiwa madhabahuni pamoja kutenga muda wa kuandaa ujumbe wa neno kabla ya kuhubiri mbele ya waumini

Hali hiyo itawaepusha kuhubiri maneno ya siasa, ndoto zao na yaliyotokana na mawazo yao.Hayo ameyasema Askofu wa Kanisa la (FPCT) Free Pentekoste Church Of Tanzania jijini Tanga Askofu Stevie Mulenga ambaye pia anachunga kanisa la FPCT Novelty, wakati akihubiri katika ibada ya jumapili iiliyofanyika katika kanisa hilo lililopo Novelty barabara ya nne mjini hapa.

  Amesema watumishi walio wengi siku hizi hawapati muda mzuri wa kuandaa neno au ujumbe na badala yake wanahubiri yaliyopo katika mawazo yao jambo ambalo ni hatari kwa maisha ya kiroho hususani kwa wale anao walisha.

Akinukuu neon kutoka kitabu cha 1Samweli 1:2,3, Yeremia 23:21-28, Amosi 8:11 na kitabu cha Yohana 1:1-3 Amesema watumishi wanatakiwa kuepuka kusimama madhabahuni kwa mazoea na badala yake wasimame wakihubiri kile ambacho Mungu amewaagiza ili kuokoa mioyo za watu ambao Mungu amewapa lakini pia kuishi maisha yenye ushuhuda mbele za Mungu na mbele za wanadamu.

No comments:

Post a Comment