HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 30 March 2015

KIGOGO WA SERIKALI ZANZIBAR ADAIWA KUCHOCHEA UGOMVI WA MASHAMBA YA EKA PEMBA.

Rais wa SMZ Dkt Ali Mohamed Sheid akichuma
karafuu zao maarufu la biashara visiwani Zainzibar



Na Masanja Mabula –Pemba
Migogoro ya ardhi inayoyahusu mashamba ya eka katika Mkoa wa Kaskazini Pemba inadaiwa kuchangiwa na mmoja wa viongozi wa juu mwenye dhamana kubwa ndani ya  Wizara ya Sheria na Katiba  Visiwani hapa .

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwepo na kiongozi mwenye dhamana katika wizara hiyo ambaye ametoa barua za kuwataka wananchi waliokabidhiwa eka na Serikali kutoyatumia mashamba hayo na kasha kuyarejesha kwa wanadaiwa kuwa walikuwa wamiliki kabla ya mapinduzi .

Baadhi ya wananchi wa Shehia ya Ukunjwi , Junguni na Limbani katika Wilaya ya Wete ,  wako njia panda juu ya matumizi ya mashamba hayo baada ya kuwekwa mabango na Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana na wananchi hao kutakiwa kutoyatumia mashamba hayo kwa shughuli za uchumi na maendeleo .

Mmoja wa wananchi Mkaazi wa Ukunjwi Ramadhaman  Ali Ramadhan  amesema kuwa kiongozi huyo amemwandikia barua na kusitisha matumizi ya shamba hilo ambalo amerithi kisheria kutoka kwa mzazi wake ambaye naye alikabidhiwa na Serikali . lakini Kamisheni imeshindwa kumlipa fidia ya mazao yake .

“Serikali ya Wilaya na Mkoa pamoja na Wizara ya Ardhi walitaka mimi niendelee kulitimia shamba hili , lakini baadaye nilipokea bara kutoka kwa Waziri wa Katiba na Sheria ikinitaka nisitishe matumizi ya shamba hili na mimi nilidai fidia ya vipando vyangu , kwa mshangao hadi leo sijalipwa ”alifahamisha .

“Baada ya kupokea barua hii shamba langu limewekwa mabango na kamisheni ya Wakfu na kuanzia siku hiyo mashamba mengine ambayo nilikuwa nimepekana nayo pia yamechukuliwa , Je , hii ndiyo azma ya Mapinduzi ? ”alihoji mwananchi huyo .

Naye Soud Abdalla Mkaazi wa Shehia ya Junguni amesema kuwa Kamisheni ya Wakfu imewekwa mabango yake kwenye shamba ambalo amelinunua baada ya kustaafu kazi , na anashangaa kuona kunajitokeza hali hiyo .
“Nilishangaa kuona mabango ya Kamisheni katika shamba langu ambalo nimelinunua kwa fedha zangui baada ya kustaafu kazi , lakini baada ya hapo sijaona mtu kudai shamba hilo kwa ni lake na mimi nasubiri atakaye chomoza  na hapo kitaeleweka ”alisisitiza Soud .

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman amekiri kuwepo na hali ya kuwekwa mabango katika mashamba ya eka pamoja na maeneo ambayo wananchi wamepimiwa viwanja na Serikali na kudai kuwa hiyi ni njama ambayo imeandaliwa na kamwe hatakubaliana nayo .

Amesema kuwa wananchi waliokabidhiwa mashamba ya eka na Serikali baada ya Mapinduzi wanapaswa kuyatunza na kuyaendeleza kwa kupanda miti ya matunda na biashara ikiwemo mikarafuu na kwamba Serikali haijatoa tamko la kuwaponya mashamba hayo .
“Mwenye mamlaka na uwezo wa kutengua matumizi ya mashamba hayo ni Rais wa Zanzibar , hivyo nawaomba wananchi kuyatunza na kuyaendelea mashamba hayo kwani Serikali bado inatambua umiliki wao kuwa ni halali ”alifahamisha .

Kitendo cha Kamisheni ya Wakfu kuweka mabango katika Mashamba hayo ambayo yalikabidhiwa wananchi baada ya mapinduzi ya januari 12, 1964 kinakinzana na azma ya mwasisi wa  Mapanduzi hayo mzee Abeid Aman Karume ya kutoa eka tatu tatu kwa wananchi wa Zanzibar .

No comments:

Post a Comment