HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 31 March 2015

ULIMWENGU ABANIWA KUONDOKA TP MAZEMBE "MADILI YA ULAYA YAPOTEZEWA"



MSHAMBULIAJI wa TP Mazembe ya DRC, Thomas Ulimwengu amesema kwamba hafurahii maisha katika klabu yake hiyo na sasa anataka kuondoka, lakini kila ofa inayokuja ‘inatiwa kapuni’.

Akizungumza na vyombo vya habari Ulimwengu, mshambuliaji mwenye nguvu, kasi na uwezo mkubwa wa kuwapita mabeki, alisema kwamba mmiliki wa klabu yao, Moise Katumbi Chapwe amekuwa akiwabania kuondoka.

“Inaniuma sana hadi sasa bado nacheza Afrika, zinakuja ofa nyingi tunatakiwa na klabu za Ulaya, lakini bosi anakataa, kisa bado tuna Mkataba na timu,”amesema Ulimwengu.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Moro United, amesema kwamba anapojaribu kwenda kumuulizia bosi wake huyo juu ya ofa hiyo amekuwa kama ‘akipotezea’.

Kuna wakati baada ya kusemea hajapata ofa ya klabu moja ambayo nilikuwa nina uhakika imefika, ikabidi niwaambie wale jamaa wanitumie mimi nimpelekee yeye mkono kwa mkono, lakini pamoja na kufanya hivyo, bado alizungua,”amesema Ulimwengu.

Mshambuliaji huyo tegemeo wa Tanzania kwa sasa amesema kwamba kwa sasa anasubiri tu kumaliza Mkataba wake mwakani, ili aangalie ustaarabu mwingine.

Lakini Ulimwengu amesema inamuuma sana katika wakati huu ambao klabu nyingi za Ulaya zinamtaka, Mazembe inambania.

“Yaani imefika wakati sikufichi ndugu yangu, nafurahi tu kwa sababu pale nakubalika, nina marafiki, mashabiki wananikubali, lakini nikifikiria kwamba napoteza nafasi za kusogea mbele, nakosa furaha kabisa,”amesema.

Pamoja na hayo, Ulimwengu amesema hakati tamaa, ataendelea kuitumikia Mazembe kwa uadilifu wa hali ya juu hadi hapo atakapomaliza Mkataba wake aondoke salama.  

No comments:

Post a Comment