HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 22 March 2015

"MAMLAKA YA MAJI PEMBA YATAKIWA KUVITAMBUA VYANZO VYA MAJI"



Na .Masanja Mabula PEMBA
Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) Kisiwani Pemba  imetakiwa kuyatambua maeneo  yote yenye  vyanzo vya  maji ili iyawekea ulinzi dhidi ya uvamizi unaofanywa na baadhi ya wananchi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba  Omar Khamis Othman wakati akizindua wa Mradi wa  maji katika Kijiji cha Chekea  Shehia ya Mtambwe Kaskazini Wilaya ya Wete  ikiwa ni  sherehe za maadhimisho ya  Wiki ya Maji Duniani .

Amesema kuwa Mamlaka inapaswa kuyawekea ulinzi maeneo yote vya vyanzo vya Maji kwa kuhakikisha kwamba inayawekea uzio ili kuziba mianya ya wananchi wanavamia maeneo kuweza kuyafikia .

Katika Hatuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa Wilaya ya Wete Bw Hassan Khatib Hassan , amewataka wananchi wa Kijiji cha Chekea Mtambwe Kaskazini kuutumia mradi huo wa maji kwa ajili kukuza uchumi na maendeleo yao na Taifa kwa Ujumla.

Mapema Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji (ZAWA) Pemba  Juma Ali Othman amesema kuwa mradi huo utaondoa changamoto ya uhaba wa maji iliyokuwa inawakabili wananchi wa Kijiji hicho .

Ameeleza kwamba Mamlaka imechimba Kisiwa katika Kijiji hicho chenye urefu wa mita 105 na kinauwezo wa kutoa lita 960 kwa siku ambapo mahitaji ya wananchi wa Kijiji hicho ni 450 kwa siku .

No comments:

Post a Comment