HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Saturday, 28 March 2015

click hapa "KUPATA TETESI ZA USAJILI MAJUU MAJIRAYA KIANGAZI"



Meneja wa Chelsea Jose Mourinho anaweza kumchukua Straika wa Tottenham Emmanuel Adebayor kwa Mkopo kwa ajili ya Msimu ujao.
Emmanuel Adebayor "mtata"
Gazeti la Uingereza Daily Mirror limeripoti kuwa Mourinho anamtaka Adebayor Stamford Bridge ili kuchukua nafasi ya Didier Drogba ambae anatafakari kustaafu mwishoni mwa Msimu.Mourinho anahitaji Straika wa 3 wa akiba ili kuchukua nafasi za Diego Costa na Loic Remy endapo wataumia au kufungiwa.

Ikiwa Adebayor atatua Chelsea hii itakuwa mara ya pili kwake na Mourinho kuungana kwani Miaka Minne iliyopita Mourinho akiwa Real Madrid alimchukua Adebayor kwa Mkopo kuziba pengo la Majeruhi Gonzalo Higuain na huko Straika huyo aling'ara na kufunga Bao 8 katika Mechi 22.Hivi sasa Adebayor, Straika kutoka Togo mwenye Miaka 31, hana namba Spurs iliyo chini ya Meneja Mauricio Pochettino.

Mwezi Januari Adebayor nusura ahamie kwa Mkopo West Ham lakini Mkuu wa Spurs, Daniel Levy, akaweka ngumu kwa kuitaka West Ham ilipe Mshahara wote wa Mchezaji huyo wakati akiwa huko kwa Mkopo kitu ambacho West Ham walikikataa.

Paul Pogba "fundi"
Zipo ripoti kuwa Manchester United itatumia zaidi ya Pauni Milioni 100 mwishoni mwa Msimu ili kuimarisha Kikosi chao.

Man United, ambao sasa wapo Nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu England nyuma ya Chelsea, Man City na Arsenal, mwanzoni mwa Msimu walitumia zaidi ya Pauni Milioni 150 kununua Wachezaji wapya wakiwemo Radamel Falcao, aliechukuliwa kwa Mkopo kutoka AS Monaco, na Angel Di Maria, ambao hawajaonyesha cheche zozote huko Old Trafford.

Ripoti zimedai sasa Van Gaal atalenga Wachezaji Vijana waliokomaa na mahiri kwenye Klabu na Timu zao za Taifa.Miongoni mwa walengwa wake waliotajwa kwenye Ripoti hiyo ni Beki wa Germany na Klabu ya Borussia Dortmund, Mats Hummels, mwenye Miaka 26, na Chipukizi wa Kimataifa wa Holland, Memphis Depay.

Wengine ni Kiungo wa France na Juventus, Paul Pogba ambae alitokea Timu ya Vijana ya Man United.Pia watajwa wengine ni Fulbeki wa FC Porto, Danilo, na yule Mbrazil wa Barcelona Dani Alves.Pia waliwahi kutajwa Garreth Bale anaesakamwa na Mashabiki wa Klabu yake Real Madrid lakini mwenyewe amesisitiza kubakia Madrid.

No comments:

Post a Comment