HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 3 December 2014

YDCP YAFANYA SHEREHE YA WATOTO YATIMA NA WALEMAVU TANGA, "WAZAZI NA WALEZI WAAASWA KUWATHAMINI"..!!



JAMII imetakiwa kuwasaidia, kuwajali na  kuwatahamini watoto yatima na walemavu kwani wanahaki ya kuishi kama watoto wengine.
Hayo ameyasema mshauri wa mradi wa kitaalum kutoka nchini Finland  Tero Tapani wakati akizungumza katika sherehe ya watoto yatima na walemavu ambayo imefanyika katika ukumbi wa mkutano YDCP Jijini Tanga.


Aidha mtu ambaye atamthamini mtoto mlemavu na kumtunza atakuwa amefanya jambo la Baraka mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
Naye Mratibu wa kituo hicho William Henry amesema kuwa lengo la kuadhimisha sikukuu hiyo ya watoto kila mwaka ni kuwaweka watoto hao pamoja ili nao wao wajisikie vizuri kama watoto wengine.

Kwa upande wake mgeni rasmi ambaye ni Mch. Wa kanisa la FPCT Free Pentekoste Of Tanzania Ayubu Kuminambili ambaye alimwakilisha makamu Askofu wa Taifa wa kanisa Stivie Mulenga amesema kuwa amdharauliye wenzake atenda dhambi bali amhurumiaye mwenzake ana heri,hivyo ni vyema kuwapenda watoto walemavu na kuwatunza kwani Mungu amewaumba kwa makusudi maalum.

No comments:

Post a Comment